Business

Wafugaji wa Nyuki Lamu Walia Kudorora kwa Biashara ya Asali Kutokana na Asali Ghushi

Published

on

Wafugaji wa nyuki katika Kaunti ya Lamu wamelalamikia kuporomoka kwa soko la asali halisi, wakilaumu kuongezeka kwa asali ghushi inayojaa sokoni.

Kwa mujibu wa wafugaji hao, baadhi ya wafanyabiashara wasio waaminifu wamekuwa wakichanganya sukari kwenye asali na kuiuza kwa bei ya chini, hali inayovuruga ushindani wa haki na kuharibu sifa ya bidhaa ya asali asilia.

Wakizungumza na vyombo vya habari, walisema kuwa biashara yao sasa inaendelea kusambaratika huku wateja wakipungua kwa kasi, wakihofia kununua bidhaa zisizo halisi. Wamekadiria hasara kubwa na kupoteza wateja waliokuwa wa kudumu.

Katika hatua ya kukabiliana na tatizo hilo, mamlaka husika zimeonya kuwa wafanyabiashara wanaouza asali ghushi watachukuliwa hatua kali za kisheria. Wametakiwa kusitisha mara moja biashara hiyo haramu inayowahujumu wakulima halali.

Aidha, wito umetolewa kwa wanunuzi kuwa waangalifu wanaponunua asali, kuhakikisha wanachukua bidhaa kutoka kwa vyanzo vinavyoaminika ili kuepuka kununua bidhaa bandia.

Leave a Reply

Your email address will not be published. Required fields are marked *

Trending

Exit mobile version