News

Vijana waitaka serikali kuzingatia sheria

Published

on

Vijana na wanaharakati wa maswala ya vijana kaunti ya Mombasa wanaitaka serikali ya kitaifa kutekeleza maswala ya msingi yanayohusu uongozi na utawala wa sasa.

Vijana hao wakiongozwa na mwenyekiti wa Nyali Youth Association Evans Mtalii walisisitiza kuwa hawataki mazungumzo bali hatua za msingi kufanyika.

Mtalii alisema serikali imekuwa ikipuuza kilio na changamoto wanazopitia vijana ikiwemo utekaji nyara, mauwaji ya kiholela na ukiukaji wa haki za kibinadamu miongoni mwa changamoto zingine.

“Hatuhitaji mazungumzo kukomesha utekaji nyara, kukomsha mauwaji ya kiholela sisi tushawaambia matatizo na changamoto ambazo tunataka serikali iangazie hivyo sio lazima watuite kwa mazungumzo rekebisheni peke yenu bila ya kutuita kwa mazungumzo”. … alisema Evans

Mtalii vile vile alisema inasikitisha kuona kwamba kuna baadhi ya viongozi wanaoyafumbia macho madhila wanayopitia vijana.

Wakati huo huo Edwin Shamiri alimsihi rais William Ruto kuhakikisha kuwa anaongoza nchi kulingana na katiba.

Shammir alisema wapo tayari kama wakereketwa kutete na kuhakikisha haki za mwananchi hazikiukwi kivyovyote vile.

Taarifa ya Elizabeth Mwende

Leave a Reply

Your email address will not be published. Required fields are marked *

Trending

Exit mobile version