News

Kanja aagizwa kuwasilisha stakabadhi za Polisi kwa NPSC

Published

on

Huduma ya kitaifa ya polisi nchini NPS iliagizwa kukabidhi orodha ya malipo ya polisi na kazi zote zinazohusiana na raslimali za umma kwa Tume ya kitaifa ya huduma ya polisi nchini NPSC.

Agizo hilo lilitolewa na Kamati ya bunge la kitaifa kuhusu uhasibu wa umma inayoongozwa na Mbunge wa Butere Tindi Mwale ambayo ilimuagiza Inspekta Jenerali wa polisi Douglas Kanja kutekeleza agizo hilo mara.

Kulingana na kamati hiyo, hatua hiyo itapunguza uhasama uliopo kati ya taasisi hizo mbili za umma huku ikimtaka Kanja kuhakikisha pia anawasilisha orodha ya mishahara sawa na kuruhusu tume hiyo kutekeleza majuku yake kwa mujibu wa katiba.

Hata hivyo Inspekta Jenerali wa polisi nchini Douglas Kanja aliahidi kutekelezwa kwa maagizo hayo huku mkurugenzi mkuu wa Tume ya huduma ya kitaifa ya polisi nchini NPSC Peter Lelei akiahidi kuandikia Kamati hiyo barua kuhakikisha iwapo maagizo hayo yametekelezwa.

Kanja alikuwa aliitwa mbele ya kamati hiyo kufuatia ripoti iliyotolewa na Mkaguzi mkuu wa hesabu za serikali Magaret Nyakang’o iliyoashiri kwamba NPSC haijaweza kutekeleza majukumu yake kwa kunyimwa stakabadhi muhimu.

Taarifa ya Mwahoka Mtsumi

Leave a Reply

Your email address will not be published. Required fields are marked *

Trending

Exit mobile version