Entertainment

Diamond Platnumz: Nilishawahi Kuoa, na Kuna Siku Nitawaambia Ikawaje

Kauli ya Diamond Platnumz kuhusu ndoa imewavuruga mashabiki mitandaoni, baada ya picha zenye taswira ya harusi kusambaa. Ingawa hajasema wazi kama ameoa, ujumbe wake wa kina kuhusu kukaa kimya na uvumilivu umeacha maswali mengi kuliko majibu. Je, Diamond ameoa kwa siri? Au ni ujanja wa kisanii?

Published

on

Kauli ya msanii nyota na mfanyabiashara mashuhuri Diamond Platnumz, iliyoambatanishwa na picha zinazodaiwa kuhusiana na ndoa ya mkeka, imewaacha mashabiki wengi katika hali ya sintofahamu—wengi wakijiuliza iwapo msanii huyo maarufu ameoa au la.

Kupitia chapisho lake katika mitandao ya kijamii, Diamond alieleza kuwa amekuwa akikwepa mahojiano na vyombo vya habari kwa makusudi, akisema kufanya hivyo kumemsaidia kuepuka maneno ya upotoshaji na uzushi kutoka kwa watu.

Akiongea kwa tafakari na kina na kwa hisia, Diamond alisema kuwa kukaa kimya wakati anakumbwa na maneno ya uongo ni jambo linalohitaji ukomavu wa hali ya juu, na kumshukuru Mungu kwa kumpa hekima hiyo:

“Miongoni mwa vitu ambavyo nimejifunza ni ukomavu wa kukaa kimya… Ukomavu huu unahitaji uvumilivu wa hali ya juu, moyo wa subira, na roho ya kukaza pale ambapo mtu au watu wanapokupaka matope kwenye jamii ilhali wewe unajua ukweli, lakini unachagua kukaa kimya. Si jambo jepesi, lakini faida yake ni kubwa – unapambana vita zako kwa msaada wa Mungu, na mwisho wake unakuwa mshindi.”

Hata hivyo, katika ujumbe huo, Diamond hakuthibitisha moja kwa moja kama kweli ameoa, licha ya picha zinazomuonesha akiwa katika mazingira yanayofanana na hafla ya harusi. Kauli yake ya mwisho nayo haikufafanua jambo hilo kikamilifu:

“Anyways: Najua kila mmoja wenu ana picha tofauti kabisa kuhusu Diamond Platnumz na KUOA, ila tu nataka leo niwaambie kuwa HUYU DIAMOND PLATNUMZ ALISHAWAHI KUOA, na kuna siku nitawaambia ikawaje,” aliandika.

Kauli hiyo imeongeza maswali miongoni mwa mashabiki, huku wengine wakichukulia comment ya Juma Jux kama ushahidi wa ndoa hiyo. Jux aliandika:

“Welcome to the team my brother 🤝”

Kumbuka kuwa mwezi huu, Diamond anatarajiwa kutangaza msanii mpya atakayesajiliwa chini ya lebo yake ya muziki WCB Wasafi, kufuatia kuondoka kwa Mbosso mapema mwaka huu.

Baadhi ya Hisia za Mashabiki:

  • Simba_Bhoy: Brother mbona ndoa ya mkeka iyoooo……………….😮

  • Msafitheswagg: HII ITAKUWA NDOTO NGOJA NIENDELEE KULALA

  • Popineshine: Sikuwahi waza kama itatokea hii miaka hii ya karibuni kwa kweli ni surprise..😱 ONGERA SIMBA🫡

  • Kimkayndo: Mimi naondoka na paragraph ya mwisho tajiri

Leave a Reply

Your email address will not be published. Required fields are marked *

Trending

Exit mobile version