Entertainment
Diamond Platnumz: Nilishawahi Kuoa, na Kuna Siku Nitawaambia Ikawaje
Kauli ya Diamond Platnumz kuhusu ndoa imewavuruga mashabiki mitandaoni, baada ya picha zenye taswira ya harusi kusambaa. Ingawa hajasema wazi kama ameoa, ujumbe wake wa kina kuhusu kukaa kimya na uvumilivu umeacha maswali mengi kuliko majibu. Je, Diamond ameoa kwa siri? Au ni ujanja wa kisanii?

Kauli ya msanii nyota na mfanyabiashara mashuhuri Diamond Platnumz, iliyoambatanishwa na picha zinazodaiwa kuhusiana na ndoa ya mkeka, imewaacha mashabiki wengi katika hali ya sintofahamu—wengi wakijiuliza iwapo msanii huyo maarufu ameoa au la.
Kupitia chapisho lake katika mitandao ya kijamii, Diamond alieleza kuwa amekuwa akikwepa mahojiano na vyombo vya habari kwa makusudi, akisema kufanya hivyo kumemsaidia kuepuka maneno ya upotoshaji na uzushi kutoka kwa watu.
Akiongea kwa tafakari na kina na kwa hisia, Diamond alisema kuwa kukaa kimya wakati anakumbwa na maneno ya uongo ni jambo linalohitaji ukomavu wa hali ya juu, na kumshukuru Mungu kwa kumpa hekima hiyo:
“Miongoni mwa vitu ambavyo nimejifunza ni ukomavu wa kukaa kimya… Ukomavu huu unahitaji uvumilivu wa hali ya juu, moyo wa subira, na roho ya kukaza pale ambapo mtu au watu wanapokupaka matope kwenye jamii ilhali wewe unajua ukweli, lakini unachagua kukaa kimya. Si jambo jepesi, lakini faida yake ni kubwa – unapambana vita zako kwa msaada wa Mungu, na mwisho wake unakuwa mshindi.”
Hata hivyo, katika ujumbe huo, Diamond hakuthibitisha moja kwa moja kama kweli ameoa, licha ya picha zinazomuonesha akiwa katika mazingira yanayofanana na hafla ya harusi. Kauli yake ya mwisho nayo haikufafanua jambo hilo kikamilifu:
“Anyways: Najua kila mmoja wenu ana picha tofauti kabisa kuhusu Diamond Platnumz na KUOA, ila tu nataka leo niwaambie kuwa HUYU DIAMOND PLATNUMZ ALISHAWAHI KUOA, na kuna siku nitawaambia ikawaje,” aliandika.
Kauli hiyo imeongeza maswali miongoni mwa mashabiki, huku wengine wakichukulia comment ya Juma Jux kama ushahidi wa ndoa hiyo. Jux aliandika:
“Welcome to the team my brother 🤝”
View this post on Instagram
Kumbuka kuwa mwezi huu, Diamond anatarajiwa kutangaza msanii mpya atakayesajiliwa chini ya lebo yake ya muziki WCB Wasafi, kufuatia kuondoka kwa Mbosso mapema mwaka huu.
Baadhi ya Hisia za Mashabiki:
-
Simba_Bhoy: Brother mbona ndoa ya mkeka iyoooo……………….😮
-
Msafitheswagg: HII ITAKUWA NDOTO NGOJA NIENDELEE KULALA
-
Popineshine: Sikuwahi waza kama itatokea hii miaka hii ya karibuni kwa kweli ni surprise..😱 ONGERA SIMBA🫡
-
Kimkayndo: Mimi naondoka na paragraph ya mwisho tajiri
Entertainment
Joy to The World! Mke wa Michael Yena, Grace Santa, Ajifungua
Mwimbaji wa Injili Michael Yena na mkewe Grace Santa wamebarikiwa na mtoto wao wa kwanza. Jua zaidi kuhusu ujio huu wa neema na wimbo mpya ‘Ametutendea’ unaosindikiza tukio hilo la kipekee!

Ni shangwe! Ni nderemo! Ni vigelegele! Baraka kubwa imetua rasmi kwenye familia changa ya mwimbaji wa nyimbo za Injili, Michael Yena, baada ya mkewe kipenzi Grace Santa kujifungua mtoto wao wa kwanza! 🍼👶
Kupitia ukurasa wake rasmi wa Facebook, Yena alipakia picha na tulipomtafuta mda mchache uliopita akathibitisha habari hiyo njema.
Kwenye Facebook, Yena, aliandika:
“We give God all the Glory. #Ametutendea”
Lakini subiri kidogo! Ikiwa unataka kujua mtoto ni wa kike au wa kiume… tafadhali kaa mkao wa kusubiri 😅. Kulotia maongezi ya njia ya simu, Yena amesema, kwa sasa jinsia ya mtoto itabaki kuwa “fiche”, wakisubiri wakati maalum wa kufanya tangazo rasmi. Hii ni kama suspense ya movie nzuri—yaani hata mtoto wao anaingia duniani na style! 🎬✨
🎶 Wimbo Mpya Wenye Maana Kubwa: “Ametutendea”
Katika kusindikiza ujio wa mtoto wao, Michael Yena ameendelea kusukuma wimbo wake mpya “Ametutendea”—na kwa kweli, jina la wimbo linazungumza moja kwa moja na tukio la maisha yao. Ni ushuhuda wao.
👉 Tazama video ya wimbo huo hapa:
🔗 Ametutendea – Michael Yena (Official Video)
Wimbo huu ni wimbo wa ushuhuda, wa shukrani, na wa imani. Ukiusikiliza huku ukijua kuwa umetoka kwa mtu ambaye ameonja wema wa Mungu kwa kiwango hiki—huwezi kubaki vilevile!
💍 Safari ya Upendo Yao
Kwa wanaofuatilia historia yao ya kimapenzi na kiroho, Michael na Grace walifunga ndoa yao mwezi Aprili mwaka 2024. Kwa kipindi kifupi, wameonyesha mfano wa ndoa yenye msingi wa maombi, heshima na maelewano. Na sasa, wameingia katika ukurasa mpya wa maisha—ukurasa wa uzazi!
Tunawatakia kila la kheri katika safari yao ya kuwa wazazi. Dunia imepata mtoto mwingine wa neema, na hakika tunaamini huyu naye atakuwa baraka kwa vizazi. Kama ilivyo kwa mashairi ya wimbo wao mpya, tunaungana nao kusema kwa nguvu zote:
“AMETUTENDEA!” 🎉
📌 Endelea kutembelea www.cocomedia.co.ke kwa habari za utendeti, matukio ya kusisimua, habari na kila kinachohusu burudani.
Entertainment
Creative Economy Forum 2025: Ruby Kache Uso kwa Uso na Bien
Ruby Kache na Bien wakutana Nairobi kwenye Jukwaa la Uchumi wa Ubunifu! 🌟

Jiji la Nairobi liling’aa zaidi wiki hii baada ya kuandaa Jukwaa la Uchumi wa Ubunifu — tukio la kipekee lililowakutanisha wabunifu, wanamuziki, na wadau wa sanaa kutoka Kenya na Marekani. Mbali na mijadala ya sera na mipango ya maendeleo, tukio hili lilikutanisha watu mashuhuri.
Mrembo wa redio, Ruby Kache, alikutana na nyota wa muziki, Bien aliyekuwa kwenye kundi la maarufu Sauti Sol!
Kwa wanaosikiliza redio, jina la Ruby Kache si geni. Ni mtangazaji machachari wa kipindi cha “The Wave” kupitia Coco FM, kinachoenda hewani kila Jumamosi kuanzia saa 4 asubuhi hadi saa 7 mchana. Kipindi chake kinajulikana kwa kuangazia maisha ya vijana, muziki wa kisasa, mitindo na mazungumzo yenye msisimko.
Katika kongamano hili, Ruby alihudhuria kama mshiriki, lakini kama ilivyo kawaida yake — aliiba spotlight bila kusema neno jukwaani. Uvaaji wake, tabasamu lake na muingiliano wake na wadau wengine ulitosha kuonyesha uwepo wake wa nguvu.
Moja ya highlights kubwa za siku hii ilikuwa ni wakati Ruby Kache alipokutana na Bien. Ruby alirekodi kipande kifupi na kukipakia kwenye ukurasa wake wa Facebook, huku mashabiki wakishangilia. Bien, nguli wa mziki anayeshikilia tuzo ya muimbaji bora Afrika Mashariki, alikuwa mgeni maarufu katika tukio hilo.
Baadhi ya waunda maudhui maarufu kutoka Pwani waliopamba hafla hiyo ni pamoja na Presenter Kai, Beka Ruga, Mwagwaya Ndani, na Princess Fynick, waliokuja kwa mitoko ya kisasa. Kwa upande wa muziki, Reagan Dandy alikuwa miongoni mwa wanamuziki wachache kutoka Pwani waliobahatika kuhudhuria tukio hilo la hadhi ya kimataifa.
Jukwaa la Uchumi wa Ubunifu limeibuka kama jukwaa muhimu kwa kuvunja mipaka kati ya sanaa, biashara na teknolojia. Kupitia mikutano kama hii, wasanii, waunda maudhui na wadau wa sekta ya ubunifu wanapata nafasi ya kuunganishwa na fursa za kimataifa, kujifunza kuhusu ulinzi wa kazi zao, na kuelewa jinsi ya kujitegemea kiuchumi kupitia vipaji vyao. Kwa kizazi kinachotegemea mitandao na ubunifu kama njia ya kujieleza, majukwaa haya yanakuwa daraja kati ya ndoto na mafanikio halisi.
Kwa washiriki kutoka Pwani na sehemu nyingine za Kenya, kongamano hili halikuwa tu mahali pa kuonekana, bali pa kujifunza, kuunganishwa na kuchochewa kufikiria ubunifu kama ajira na biashara. Uwepo wa majina maarufu kama Ruby Kache, Bien, na waunda maudhui wengine wakubwa ulitoa motisha kwa vijana, huku ikithibitisha kuwa sanaa inaweza kuwa nguvu ya kiuchumi na chombo cha mabadiliko chanya katika jamii.