News

JSC, yashutumu mashambulizi dhidi ya Idara ya Mahakama

Published

on

Tume ya huduma za Mahakama nchini JSC imeshtumu vikali tabia inayoendelea kusheheni nchini ya kuwashambulia hadharani majaji kuhusu uamuzi wanaoutoa wa dhamana kwa washukiwa wa kesi za maandamano.

Katika taarifa iliyotolewa na JSC kupitia Katibu wa Idara wa Tume hiyo Winfridah Mokaya, ilisema tume hiyo imeonyesha wasiwasi mkubwa kuhusu athari za maamuzi ya hivi majuzi yaliyotolewa na Mahakama ya Nanyuki.

Katika Mahakama hiyo zaidi ya watu 100 waliokamatwa kutokana na maandamano ya Julai 7 katika kaunti ya Laikipia waliachiliwa kwa dhamana ya shilingi elfu 50 pesa taslimu kila mmoja baada ya kushtakiwa kwa uharibifu wa mali.

“Tunashangazwa na tabia ya kuwashambulia majaji hadhara kuhusu uamuzi wanaotoa kuhusu washukiwa wa maandamano ya Juni 25 na Julai 7 wakati wa maandamano ya Sabasaba na Mahakama iko kisheria na inafuata sheria”, alisema Mokaya.

Winfridah ambaye pia ni Msajili mkuu wa Idara ya Mahakama nchini amesema wakosoaji akiwema Jaji mkuu wa zamani David Maraga ambao wanashinikiza kuondolewa kwa mashtaka ya ugaidi dhidi ya waandamanaji, akisema wanafaa kuheshimu mahakama.

Wakati huo huo ameonya kwamba mashambulizi dhidi ya idara ya Mahakama huenda yakasambaratisha shughuli za kupatikana haki kwa wananchi.

Taarifa ya Mwahoka Mtsumi

Leave a Reply

Your email address will not be published. Required fields are marked *

Trending

Exit mobile version