Connect with us

News

JSC, yashutumu mashambulizi dhidi ya Idara ya Mahakama

Published

on

Tume ya huduma za Mahakama nchini JSC imeshtumu vikali tabia inayoendelea kusheheni nchini ya kuwashambulia hadharani majaji kuhusu uamuzi wanaoutoa wa dhamana kwa washukiwa wa kesi za maandamano.

Katika taarifa iliyotolewa na JSC kupitia Katibu wa Idara wa Tume hiyo Winfridah Mokaya, ilisema tume hiyo imeonyesha wasiwasi mkubwa kuhusu athari za maamuzi ya hivi majuzi yaliyotolewa na Mahakama ya Nanyuki.

Katika Mahakama hiyo zaidi ya watu 100 waliokamatwa kutokana na maandamano ya Julai 7 katika kaunti ya Laikipia waliachiliwa kwa dhamana ya shilingi elfu 50 pesa taslimu kila mmoja baada ya kushtakiwa kwa uharibifu wa mali.

“Tunashangazwa na tabia ya kuwashambulia majaji hadhara kuhusu uamuzi wanaotoa kuhusu washukiwa wa maandamano ya Juni 25 na Julai 7 wakati wa maandamano ya Sabasaba na Mahakama iko kisheria na inafuata sheria”, alisema Mokaya.

Winfridah ambaye pia ni Msajili mkuu wa Idara ya Mahakama nchini amesema wakosoaji akiwema Jaji mkuu wa zamani David Maraga ambao wanashinikiza kuondolewa kwa mashtaka ya ugaidi dhidi ya waandamanaji, akisema wanafaa kuheshimu mahakama.

Wakati huo huo ameonya kwamba mashambulizi dhidi ya idara ya Mahakama huenda yakasambaratisha shughuli za kupatikana haki kwa wananchi.

Taarifa ya Mwahoka Mtsumi

Continue Reading
Click to comment

Leave a Reply

Your email address will not be published. Required fields are marked *

News

Waziri wa zamani Dalmas Otieno Afariki

Published

on

By

Mbunge wa zamani wa eneo bunge la Rongo Dalmas Otieno ameaga dunia.

Kiongozi huyo shupavu na mweledi katika uzungumzaji, ameaga dunia Septemba 7, 2025 nyumbani kwake katika mtaa wa Kileleshwa jijini Nairobi.

Marehemu ambaye aliwahi shikilia Wizara mbalimbali nchini pamoja na taasisi za umma muhimu kuanzia utawala wa Rais wa pili nchini Hayati Daniel Arap Moi katika miaka ya 80 atakumbukwa na wengi kwa mchango wake nchini.

Taarifa za Kifo chake zimetolewa na mwanawe Eddy Otieno.

Otieno alichaguliwa kwa mara ya kwanza kuingia bungeni na kuwaakilisha eneo bunge la Rongo mnamo mwaka 1988, na kisha baadaye kuhudumu kama Waziri wa ustawi wa viwanda kati ya 1988-1991.

Mwaka wa 1991 aliteuliwa kuwa Waziri wa Leba, lakini pia akahudumu kama Waziri uchukuzi na mawasiliano chini ya utawala wa Rais Daniel Toroitich Arap Moi.

Viongozi mbalimbali wakiongozwa na Spika wa bunge la kitaifa Moses Wetangula wametaka Mwendazake kama kiongozi alichagia mengi nchini hasa suala zima la maendeleo na miswada muhimu bungeni.

Mungu ailaze roho yake pema Peponi.

Taarifa ya Eric Ponda

Continue Reading

News

Baraza la vyombo vya habari MCK lakerwa na baadhi ya vyombo habari

Published

on

By

Baraza la vyombo vya habari nchini MCK limeeleza kusikitishwa na hatua ya baadhi ya vyombo vya habari nchini kumwingilia rais wa chama cha mawakili LSK Faith Odhiambo baada ya kukubali kujumuishwa kwenye kamati ya kuangazia fidia kwa waathiriwa wa maandamano nchini.

MCK ilisema hatua ya Odhiambo kujumuishwa katika kamati hiyo kuhakikisha waathiriwa wa maandamano hayo wanapata haki kwa mujibu wa sheria.

Katika taarifa kwa vyombo vya habari, baraza hilo lilipongeza juhudi za vyombo vya habari kwa kuangazia kwa undani maandamano yaliyofanyika nchini na hata baadhi ya wanabari kujitokeza kutoa ushahidi mahakamani.

MCK ilisema hatua ya baadhi vyombo vya habari kukosoa mwelekeo wa Odhiambo kunaiweka LSK katika hatari ya ukosoaji zaidi, katika juhudi za kuangazia usawa kwenye maswala ya uongozi dhabiti nchini.

Taarifa ya baraza la vyombo vya habari nchini MCK.

Ilieshinikiza wakenya kufahamu kuwa chama cha LSK kinaongozwa na taasisi muhimu za umma ikiwepo idara ya mahakama, ofisi ya mkurugenzi mkuu wa mashtaka ya umma, ofisi ya mkuu wa sheria nchini vile vile tume ya malalamishi kwa vyombo vya habari.

MCK ilivitaka vyombo vya habari kumruhusu Odhiambo kuendelea kutekeleza majukumu yake bila muingilio katika kamati hiyo.

Taarifa ya Joseph Jira

Continue Reading

Trending