News
Ethekon: Uchaguzi mkuu utakuwa huru na haki, 2027
Tume huru ya uchaguzi na mipaka nchini IEBC imewahakikishia wakenya kwamba uchaguzi mkuu wa mwaka wa 2027 kutakuwa huru na wa haki kwani tume hiyo imejipanga kikamilifu.
Mwenyekiti wa Tume hiyo Erastus Ethekon aliyataka mashirika mbalimbali ya kijamii kushirikiana ili kuhakikisha uchaguzi huyo unakuwa huru na haki.
Akizunguza katika kongamano lililowaleta pamoja washikadau mbalimbali mjini Mombasa, Ethekon aliwahimiza vijana na waundaji maudhui mitandaoni kupeperusha habari za ukweli ili kuepuka taharuki miongoni mwa jamii.
“Nawahimiza baadhi yenu muwe makini hawa ambao ni Wananbloga kulingana na athari wako naye wakati wa uchaguzi na tusikubali kutumiwa vibaya kwa ajali ya michakato ya kidemokrasia,” alisema Ethekon.
Kwa upande wake Naibu Mwenyekiti wa Tume ya IEBC Fahima Abdallah alihimiza amani kwa jamii, akisema kupiga kura ni haki ya kila mkenya na ni muhimu kutekeleza suala hilo bila vurugu.
Taarifa ya Mwanahabari wetu