News
Serikali kukabiliana na magenge ya uhalifu nchini
Waziri wa Usalama Kipchumba Murkomen ameonya kuhusu kuongezeka kwa magenge ya wahalifu nchini.
Akizungumza katika kongamano la Jukwaa la Usalama kaunti ya Vihiga, Waziri Murkomen alitoa wito kwa inspekta jenerali wa polisi kutuma vikosi zaidi vya dharura eneo hilo ili kuwasambaratisha wahalifu hao.
Magenge ya wahalifi yamekuwa yakiripotiwa kuhangaisha usalama na maisha ya wakaazi katika sehemu mbali mbali nchini ikiwepo kaunti za hapa Pwani.
Kwa upande wake gavana wa kaunti ya Kilifi Gedion Mung’aro aliahidi kushirikiana kwa karibu na maafisa wa usalama kukomesha magenge ya wahalifu yanayowahangaisha wakaazi maarufu mawoza.
Akizungumza mjini Malindi katika kaunti ya Kilifi kwenye mkutano na vijana wa eneo hilo, gavana Mung’aro alisema serikali yake haitawavumilia vijana waliopotoka kimaadili wanaoendelea kuwahangaisha wananchi.
Wakati huohuo aliwaonya baadhi ya maafisa wa kaunti wanaowahangaisha wakaazi hususan wahudumu wa bodaboda.
Taarifa ya Joseph Jira.