Business

Biashara zadorora mjini Kilifi kufuatia likizo ya Chuo Kikuu

Published

on

Wafanyibiashara mjini Kilifi kaunti ya Kilifi wanalalamikia kushuka kwa kiwango cha biashara mjini Kilifi baada ya wateja wanaowategemea kuanza likizo.

Kulingana na uchunguzi ulifanywa na Coco Fm, wafanyibiashara wengi wa nguo kuukuu mjini Kilifi wanasema kwamba uchumi wao umeshuka kwa kiwango kikubwa tangu wanafunzi wa chuo kikuu cha Pwani kuenda likizo, hivyo kuathiri biashara zao.

Wakizungumza na cocofm wafanyibiashara hao wanasema kuwa uchumi wa kaunti ya kilifi huchangiwa pakubwa na idadi ya wanafunzi katika chuo hicho na wakati wanapokwenda likizoni basi biashara nyingi za mji wa Kilifi huanza kudorora.

Aidha wafanyibishara hao wametaja kupanda kwa gharama ya maisha kumechangia pia kudorora kwa biashara zao huku wakitoa wito kwa serikali kuu kuweka mikakati ya kupunguza gharama ya maisha.

“Kwa sasa matumizi ya pesa kaunti ya Kilifi imepungua yaani hakuna pesa hali ambayo inaathiri biashara kwani biashara nyingi zinategemea wanafunzi wa chuo kikuu cha pwani na kwa sasa wako likizo”, walisema wafanyibiashara hao.

Leave a Reply

Your email address will not be published. Required fields are marked *

Trending

Exit mobile version