News

Kongamano la kukomesha visa vya dhuluma za kijinsia Taita Taveta

Published

on

Idara ya usalama kaunti ya Taita taveta imeandaa kongamano maalum ili kujadili namna ya kukomesha visa vya dhuluma za kijinsia na kingono kaunti hiyo.

Kongamano hilo limefanyika katika eneo la Werugha, eneo bunge la Wundanyi kaunti ya Taita Taveta na limejumuisha maafisa wakuu wa serikali ya kaunti hiyo, viongozi wa kijamii pamoja na wananchi.

Kamishna wa kaunti ya Taita Taveta Josephine Onunga alibainisha kuwa kuna ongezeko la visa 186 ndani ya miaka miwili, eneo bunge la Taveta likirekodi visa 64 huku Wundanyi ikirekodi 38 hivyo kuwataka wakaazi kushirikiana na idara mbalimbali za usalama ili kukomesha visa hivyo.

“Tunapendekeza ushirikiano mkubwa zaidi na zaidi kuanzia mashinani kila boma tulindane, tujuliane hali, hakikisha unamlinda mwenzako”, alisema Onunga.

Kwa upande wao Wanaharakati wa kupambana na dhuluma za kijinsia wakiongozwa na Mary Mgola walieleza hofu yao kutokana na ongezeko la visa hivyo hasa maeneo ya mashinani.

Walisema ukosefu wa mashahidi wa kutosha wakati kesi hizo zinapowasilishwa Mahakamani, ikitajwa kama changamoto kuu wakati wa kusuluhisha kesi hizo.

Mgola aliitaka Mahakama kuhakikisha wanatoa ulinzi wa kutosha kwa mashahidi wa kesi za dhuluma za kijinsia na kingono.

Taarifa ya Elizabeth Mwende

Leave a Reply

Your email address will not be published. Required fields are marked *

Trending

Exit mobile version