News
Mboko: Serikali lazima ikomeshe mauaji dhidi ya Wanawake
Mbunge wa Likoni Mishi Mboko ameitaka serikali kuhakikisha inakomesha mauaji ya kiholela na unyanyasaji wa kingono dhidi ya Wanawake nchini.
Akizungumza na Wanahabari, Mishi alisema ni jambo la kusikitisha na kuhuzunisha kuona Wanawake wakiendelea kuuawa kila uchao na katika mazingira ya kutatanisha pasi na hatua zozote za kisheria kuchukuliwa dhidi ya wahusika.
Mbunge huyo aliitaka serikali kuongeza ufadhili kwa Muungano wa Wabunge Wanawake ili kuwawezesha kufanikisha kampeni ya kuhamasisha kwa umma dhidi ya ukatili wa kijinsia.
“Ni lazima visa kama hivi vikomeshwe, tumechoka na mauaji ya kila mara ya wanawake nchini na sisi pia tuko na haki ya kuishi na tunaiambia serikali kupitia bunge itenge pesa kupitia muungano wa wabunge wanawake ili kuelimisha jamii kuhusu kukomesha mauaji ya wanawake nchini”, alisema Mishi.

Mbunge wa Likoni na Wanawake wakipinga mauaji ya kiholela dhidi ya wanawake
Wakati huo huo aaliwataka maafisa wa usalama kushika doria kikamilifu hasa katika maeneo yanayokumbwa na visa vya ukatili dhidi ya wanawake huku akipendekeza mashirika yasiokuwa ya kiserikali kushirikiana na viongozi katika juhudi za kukomesha visa hivyo.
Taarifa ya Mwanahabari wetu