Business
Biashara zadorora mjini Kilifi kufuatia likizo ya Chuo Kikuu

Wafanyibiashara mjini Kilifi kaunti ya Kilifi wanalalamikia kushuka kwa kiwango cha biashara mjini Kilifi baada ya wateja wanaowategemea kuanza likizo.
Kulingana na uchunguzi ulifanywa na Coco Fm, wafanyibiashara wengi wa nguo kuukuu mjini Kilifi wanasema kwamba uchumi wao umeshuka kwa kiwango kikubwa tangu wanafunzi wa chuo kikuu cha Pwani kuenda likizo, hivyo kuathiri biashara zao.
Wakizungumza na cocofm wafanyibiashara hao wanasema kuwa uchumi wa kaunti ya kilifi huchangiwa pakubwa na idadi ya wanafunzi katika chuo hicho na wakati wanapokwenda likizoni basi biashara nyingi za mji wa Kilifi huanza kudorora.
Aidha wafanyibishara hao wametaja kupanda kwa gharama ya maisha kumechangia pia kudorora kwa biashara zao huku wakitoa wito kwa serikali kuu kuweka mikakati ya kupunguza gharama ya maisha.
“Kwa sasa matumizi ya pesa kaunti ya Kilifi imepungua yaani hakuna pesa hali ambayo inaathiri biashara kwani biashara nyingi zinategemea wanafunzi wa chuo kikuu cha pwani na kwa sasa wako likizo”, walisema wafanyibiashara hao.
Business
Wahudumu wa Uchukuzi Kilifi Walia na Kupanda kwa Bei ya Mafuta

Siku moja baada ya mamlaka ya udhibiti wa kawi nchini, EPPRA kutangaza kupandishwa kwa bei ya mafuta, sekta ya uchukuzi katika kaunti ya Kilifi inaelezea hofu ya kuathirika kwa biashara zao.
Wahudumu wa tuktuk,teksi, bodaboda na magari ya usafiri wa umma hapa mjini Kilifi wanasema kupanda kwa bei ya petrol na diseli kutaathiri pakubwa sekta hiyo ya uchukuzi.
Sasa wanasema kuwa watalazimika kuongeza nauli kwa abiria kutokana na gharama ya mafuta.
Ni hali ambayo imeathiri wakaazi ambao wanatarajiwa kutumia vyombo hivyo vya usafiri wakisema kuwa watalazimika kutembea kwa mguu kwa safari fupi fupi katika utekelezaji wa shughuli zao za kawaida.
Hatahivyo wametoa wito kwa serikali kuhakikisha kuwa inaingilia kati ili kuona kwamba bei za mafuta zinadhibitiwa.
Haya yamejiri huku lita moja ya mafuta aina ya petrol kaunti ya KIlifi ikiuzwa kwa shilingi 183.88 huku diseli ikiuzwa kwa shilingi 169.16 kila lita.
Lita moja ya mafuta ya taa inauzwa kwa shilingi 153.29.
Business
Uhusiano wa Kibiashara kati ya Kenya na Ufaransa Waonyesha Ukuaji Chanya

Takwimu za kibiashara kati ya kenya na ufaransa katika kipindi cha miezi mitatu ya mwisho wa mwaka 2024 zinaonyesha kuwa ufaransa ilileta humu nchini bidhaa za thamani ya shilingi bilioni 6.5 na kuagiza bidhaa za thamani ya shilingi bilioni 5.7 kutoka humu nchini hali iliyoleta uwiano bora wa kibiashara kati ya nchi hizi mbili.
Nchi hiyo sasa inalenga kuimarisha zaidi uhusiano wake na kenya ambapo kenya imewaalika waekezaji zaidi kutoka nchini ufaransa kuekeza katika sekta kadhaa za kenya.
Waziri mwenye mamlaka makuu Msalia Mdavadi anasema ufaransa inalenga sekta za kawi, miundomsingi na tekinolojia ili kuongeza biashara kati yake na kenya.