News

Alubbe: Tutazuru kaunti za Pwani kushughulikia suala tata la ardhi

Published

on

Mkurugenzi mkuu wa shirika la utetezi wa haki za ardhi nchini Kenya Land Alliance Faith Alubbe amesema wameanzisha mchakato wa kuzuru kaunti zote 6 za pwani kuangazia suala tata la mizozo ya ardhi.

Akizungumza mjini Kilifi, Alubbe alisema kwamba ukanda wa Pwani ni mojawapo ya maeneo humu nchini ambayo yamesheheni dhulma za kihistoria kwenye masuala ya umiliki wa ardhi.

Alubbe ambaye pia ni Wakili wa masuala ya ardhi alihoji kwamba mikakati yao katika mchakato huu ni kuhakikisha kuwa wapwani wanaelewa kwa kina haki zao kuhusiana na umiliki wa ardhi za kibinafsi lakini pia za kijamii.

“Kuna hazina ya ardhi ambayo ilibuniwa baada ya mswada kuhusiana na hazina hiyo kupitishwa. Rais William Ruto tayari aliwekeza fedha kwenye hazina hiyo ila idadi kubwa ya wakaazi wa pwani hawana ufahamu kuhusu hazina hiyo” alisema Alubbe.

Alubbe alisema kuwa watahakikisha kuwa wapwani wanapata hamasa za kutosha kuhusiana na suala hilo lakini pia haki zao za ardhi kwa jumla.

“Inaweza kuwa muhimu watu wa pwani kuambiwa kuhusu hii hazina, ili wakapate kuelewa ni vipi hazina hizi zinawahusu”, aliongeza Alubbe.

Taarifa ya Hamis Kombe

Leave a Reply

Your email address will not be published. Required fields are marked *

Trending

Exit mobile version