News

Chahale, aishutumu serikali kutokana na dhulma za kijinsia

Published

on

Mkurugenzi mkuu wa Shirika la kutetezi haki za kibinadamu la International Justice Mission, IJM, Vincent Chahale ameishutumu serikali kwa kuzembea katika kukabiliana na dhulma dhidi ya wasichana na wanawake nchini.

Chahale alisema kwamba wasichana wadogo wamekuwa wakidhulumiwa kingono na wengi wao huishia kukosa haki.

Alirejelea kisa ambapo msichana wa umri wa miaka 17 kwa jina Farida Julius Changawa aliyeuawa kinyama kwa kudungwa kesu eneo la Msumarini kaunti ya Kilifi ambali alisema ni sharti serikali iwe ange katika kuhakikisha kwamba wasichana wanalindwa dhidi ya dhulma katika jamii.

“Kuna pengo katika jamii yetu ambapo wasichana wadogo wanaendelea kudhulumiwa bila kupata haki. Kesi kama ya Farida ni kesi ya kusikitisha sana na tutaifuatilia hadi pale familia yake itakapopata haki” alisema Chahale.

Akiunga mkono kauli hiyo, Aggrey Juma meneja msimamizi wa Shirika la international Justice Mission alisema serikali inapaswa kutilia mkazo suala la dhulma dhidi ya Wanawake akieleza kusikitishwa na mauaji ya kinyama aliyotekelezewa marehemu Farida Julius.

Wawili hawa waliyasema haya wakati wa mazishi ya mwendazake Farida yaliyofanyika eneo la Mavueni siku Jumamosi ya tarehe ya 21 mwezi Juni 2025.

Farida alipitia dhulma ya kubakwa akiwa na umri wa miaka 13 kudhulimiwa tena miaka minne baadaye ambapo aliishia kuuawa kwa kudungwa kisu hivi majuzi.

Marehemu aliacha mtoto mmoja wa kiume mwenye umri wa miezi 9.

Taarifa ya Hamis Kombe

Leave a Reply

Your email address will not be published. Required fields are marked *

Trending

Exit mobile version