News
Wakaazi wa Lamu Waandamana Kupinga Mradi wa Kawi ya Mawe
Wakaazi wa kaunti ya Lamu kwa ushirikiano na Shirika la kijamii la Save Lamu wamefanya maandamano ya amani kupinga mradi wa uzalishaji wa Kawi ya Mawe yaani Coal Plant katika kaunti hiyo.
Wakaazi hao wamesema baada ya kufanya utafiti kuhusu mradi huo wamebaini kwamba una madhara mengi kwa afya ya jamii, wakishikilia kwamba wataendelea kuupinga mradi huo wa serikali.
Wakaazi hao aidha wameitaka Mahakama ya kuu ya Malindi ambayo inatarajiwa kutoa uamuzi wake kuhusu mradi huo kusikiliza kilio cha wakaazi wa kaunti ya Lamu na kupiga marufuku ujenzi wa mradi huo.
Hata hivyo Wawekezaji wa mradi huo ambao ni Lamu Coal Power Plant wamewasilisha rufaa Mahakamani kabla ya uamuzi wa Mahakama siku ya Alhamis.