Connect with us

News

Wakaazi wa Lamu Waandamana Kupinga Mradi wa Kawi ya Mawe

Published

on

Wakaazi wa kaunti ya Lamu kwa ushirikiano na Shirika la kijamii la Save Lamu wamefanya maandamano ya amani kupinga mradi wa uzalishaji wa Kawi ya Mawe yaani Coal Plant katika kaunti hiyo.

Wakaazi hao wamesema baada ya kufanya utafiti kuhusu mradi huo wamebaini kwamba una madhara mengi kwa afya ya jamii, wakishikilia kwamba wataendelea kuupinga mradi huo wa serikali.

Wakaazi hao aidha wameitaka Mahakama ya kuu ya Malindi ambayo inatarajiwa kutoa uamuzi wake kuhusu mradi huo kusikiliza kilio cha wakaazi wa kaunti ya Lamu na kupiga marufuku ujenzi wa mradi huo.

Hata hivyo Wawekezaji wa mradi huo ambao ni Lamu Coal Power Plant wamewasilisha rufaa Mahakamani kabla ya uamuzi wa Mahakama siku ya Alhamis.

Continue Reading
Click to comment

Leave a Reply

Your email address will not be published. Required fields are marked *

News

Rais Ruto amewaongoza wakenya kuadhimisha sherehe za Madaraka za 62

Published

on

By

Rais William Ruto amewaongoza wakenya katika kuadhimisha sherehe za Madaraka za 62 tangu taifa lijipatie uhuru.

Katika maadhimisho hayo ambayo yamefanyika katika uwanja wa Raila Odinga kaunti ya Homabay, Rais Ruto amesema taifa limepiga hatua kidemokrasia na maendeleo tangu lijipatie uhuru.

Kiongozi wa taifa ametoa changamoto kwa wakenya kuhakikisha wanaweka kipau mbele masuala ya kutekeleza mabadiliko yanayoleta ufanisi wa Taifa.

Wakenya washeherekea Madaraka, Homabay

Naye Naibu rais Prof Kithure Kindiki amemhakikishia Rais Ruto kuwa ataendelea kushirikiana naye katika kuunganisha taifa huku akimtaja Kinara wa Chama cha ODM Raila Odinga kama kiongozi aliyechangia zaidi mshikamano wa taifa.

Kwa upande wake Kinara wa Chama cha ODM Raila Odinga amemtaka Rais Ruto kuhakikisha serikali inafidia familia za wakenya walipoteza wapendwa wao wakati wa Maandamano ya vijana wa Gen Z mwezi Juni mwaka jana.

Kauli mbiu ya maadhimisho ya sherehe za mwaka huu ni “uchumi wa sanawati na maswala ya bahari”, huku ikilenga kuangazia fursa za kiuchumi zinazotokana na raslimali ya maji.

Continue Reading

News

Achani: Kaunti ya Kwale imepiga hatua katika uchumi samawati.

Published

on

By

Gavana wa kaunti ya Kwale Fatuma Achani amesema kaunti ya Kwale imepiga hatua katika kuimarisha sekta ya uvuvi na uchumi samawati.

Gavana Achani ameihimiza serikali ya kitaifa kuhakikisha inawekeza zaidi katika masuala ya uchumi samawati hasa kupitia bandari ya Shimoni, akisema itafungua ajira kwa vijana na kuboresha uchumi wa kaunti.

Akizungumza wakati wa maadhimisho ya sherehe za 62 za Madaraka katika eneo la Kinango, Gavana Achani amesema bandari ndogo 9 katika kaunti hiyo zimeboreshwa na vifaa vya kisasa ili kuchangia uhifadhi wa samaki.

Maadhimisho ya sherehe za Madaraka eneo la Kinango

Hata hivyo Viongozi waliohudhuria sherehe hizo katika gatuzi dogo la Kinango wakiongozwa na Mbunge wa Kinango Gonzi Rai, wamesisitiza haja ya viongozi pamoja na wananchi kumuunga mkono Rais Ruto katika kufanikisha ajenda ya maendeleo.

Kwa upande wake Kamishna wa kaunti hiyo Stephen Orinde amesisitiza umuhimu wa wakenya kuunga mkono miradi ya serikali hasa uchumi samawati na masuala ya bahari ili kupiga hatua kimaendeleo.

Continue Reading

Trending