News

Kuna ongezeko la visa vya wanaume kukosa nguvu za kiume eneo la Malindi

Published

on

Idara ya afya eneo bunge la Malindi kaunti ya kilifi imeripoti ongezeka la visa vya tatizo la ukosefu wa nguvu za kiume miongoni mwa wanaume katika jamii eneo hilo.

Akizungumza na Coco Fm, mtaalamu wa afya ya uzazi katika hospitali kuu ya mji wa Malindi Daktari Sudi Mohamed, amesema visa hivyo vimethibitishwa kutoka kwa baadhi ya wanaume ambao wamekuwa wakitafuta matibabu ya afya ya uzazi hospitalini humo.

Daktari Mohamed amesema hali hiyo imekuwa ikiathiri uwezo wa wanawake wengi kupata ujauzito katika jamii na hivyo kuathiri ndoa nyingi.

Aidha Daktari Mohamed amesistiza haja ya jamii kuhamasishwa zaidi kuhusu afya ya uzazi kama njia mojawapo ya kutatua tatizo la uzazi miongoni mwa wanandoa katika jamii.

Leave a Reply

Your email address will not be published. Required fields are marked *

Trending

Exit mobile version