News

Tiketi za Mashemeji Debi Zimeanza Kuuzwa

Published

on

Debi la mashemeji kati ya mahasimu wa tangu jadi kilabu ya Gor Mahia na Afc leopards siku ya jumapili kuendelea kama ilivyopangwa haya ni kwa mujibu wa waandalilizi wa mtananga huo Gor.

Tiketi za mchuano huo tayari zimetolewa ambapo mashabiki wa kawaida wanalipia ada ya shilingi shs.300 na mashabiki mashuhuri shs.500.

Awali kulikua na hali ya sintofahamu kuhusiana na ubora wa uwanja wa Kasarani ambao bado unakarabatiwa kuanda mechi ila wakilishi wa kogalo wamepata hakikisho kutoka kwa wasimamizi wa uga huo.

Katika mechi ya mkondo wa kwanza timu hizo mbili ziliisha sare tasa ugani Nyayo,Kogalo kwa sasa ni ya tatu ligini na alama 51 huku Afc Leoprads wakiwa ya sita na alama 42 kutokana na mechi 29.

Leave a Reply

Your email address will not be published. Required fields are marked *

Trending

Exit mobile version