News

Gavana Godhana Awataka Wakulima na Wafugaji Kudumisha Amani

Published

on

Gavana wa kaunti ya Tana River Dhado Godhana amezitaka jamii za wakulima na wafugaji kuzika tofauti zao na kuishi kwa Amani na umoja ili kufungua fursa zaidi za waekezaji kuingia katika kaunti hiyo.

Godhana amesema mvutano uliopo baina ya jamii hizo mbili huenda ukaibua suala la ukosefu wa usalama huku akisema kuwa hakuna mwekezaji atakayekubali kuwekeza mahali palipo na mvutano au ukosefu wa uwiano.

Aidha ameongeza kuwa suala la ardhi ambalo limekuwa donda sugu katika kaunti hiyo wanalifahamu na kama viongozi wanatafuta mbinu za kuhakikisha mzozo huo unadhibitiwa kikamilifu.

“Hii malumbano yenu mko nayo ya ardhi tunajua mna tatizo la ardhi iwe ya malisho au ukulima, tunataka tuwahimize kwamba hayo mambo mtafute njia za kudhibiti yasipite kiwango kwa sababu hakuna mtalii atakuja akijua kuna mizozo”, alisema Godhana

Leave a Reply

Your email address will not be published. Required fields are marked *

Trending

Exit mobile version