Business

Wakulima wa Mwani Kwale Waitaka Serikali Kulitambua Zao Lao

Published

on

Washikadau wa sekta ya kilimo cha mwani katika Kaunti ya Kwale wametoa wito kwa serikali kuu kulitambua rasmi zao hilo kama zao la kibiashara, ili kuwasaidia wakulima kunufaika zaidi kiuchumi.

Mshirikishi wa mradi wa mwani katika shirika la Plan International, Bw. Alfred Rono, amesema kuna haja ya kuundwa kwa sera mahsusi zitakazowalinda na kuwawezesha wakulima wa mwani kupata masoko ya uhakika na kuongeza thamani ya mazao yao.

Akizungumza katika eneo la Mkunguni, Msambweni, Bw. Rono amesema mwani una uwezo mkubwa wa kuchangia mapato ya wakulima wadogo na kukuza uchumi wa eneo hilo iwapo utawekewa mazingira wezeshi ya uzalishaji na usambazaji.

Kauli yake imeungwa mkono na Naibu Mkurugenzi wa Taasisi ya Utafiti wa Masuala ya Bahari na Uvuvi (KMFRI), Bw. Anthony Nzioka, ambaye ametoa wito kwa serikali kuu kulijumuisha zao la mwani katika orodha rasmi ya mazao ya kibiashara nchini.

Leave a Reply

Your email address will not be published. Required fields are marked *

Trending

Exit mobile version