News

ODM yapinga barua ya Orengo kujiuzulu

Published

on

Chama cha ODM kimepinga barua inayosambaa mitandaoni ikidai gavana wa kaunti ya Siaya James Orango amejiuzulu wadhifa wake.

Barua hiyo ilidaiwa kutoka kwa gavana Orengo na kuelekezwa kwa spika wa bunge la kaunti ya Siaya, pamoja na naibu gavana, baraza la magavana pamoja na kinara wa ODM Raila Odinga.

Kupitia mtandao wa X chama cha ODM kimechapisha kuwa kinauhakika barua hiyo sio sahihi na kuwataka watu kuipuuza.

Katika barua hiyo, kilichoangaziwa ni hali ya afya ya Orengo kama chanzo cha kujiuzulu, hali ambayo imedaiwa kutekelezwa kwa majadiliano na familia yake.

Barua ya kupotosha inayosambaa mtandaoni kuhusu gavana James Orengo kujiuzulu.

Orengo amekosa kuonekana hadharani kwa majuma kadhaa hali inayoibua wasiwasi miongoni mwa wakaazi anaowawakilisha.

Taarifa ya Joseph Jira

Leave a Reply

Your email address will not be published. Required fields are marked *

Trending

Exit mobile version