Business

Wakulima 9,500 Kwale Kunufaika na Mavuno Bora Baada ya Kupokea Mbegu za Kisasa

Published

on

Wakulima zaidi ya 9,500 katika Kaunti ya kwale hasa katika maeneo kame ya Kinango na LungaLunga wanatarajia mavuno zaidi ya mahindi, pojo na kunde, kufuatia serikali ya kaunti hiyo kuwasambazia mbegu za kisasa.

Kupitia idara ya kilimo na ufugaji, wakulima hao wamepokea mbegu hizo pamoja na mbolea ya bei nafuu ili kuendeleza kilimo hasa wakati huu ambapo mvua bado zinaendelea kushuhudiwa maeneo mengi nchini.

Kufikia sasa kaunti hiyo imesambaza tani 206 za mbegu, tani zaidi ya 1,000 za mbolea ya bei nafuu pamoja na matingatinga.

Hatua hiyo inatarajiwa kuongeza mapato na kuinua uchumi wa eneo hilo.

“Sai tunatarajia mavuno zaidi kufuatia hatua ya serikali ya kaunti kutusaidia na mbegu za kisasa na mbolea ya bei nafuu

Leave a Reply

Your email address will not be published. Required fields are marked *

Trending

Exit mobile version