News
Wahadhiri watishia kushiriki mgomo wa kitaifa
Muungano wa Wahadhiri wa vyuo vikuu nchini UASU umetoa matakaa ya siku 7 kwa serikali kutimiza matakwa yao la sivyo watishiriki mgomo wa kitaifa.
Wahadhiri hao walisema iwapo serikali itaendelea kukaidi suala hilo basi watasambaratisha shughuli za masomo ya vyuo vikuu 41 kote nchini.
Muungano huo wa UASU, uliilaumu serikali kwa kushindwa kutekeleza makubaliano ya pamoja nyongeza ya mishahara ikiwemo malimbikizi ya shilingi bilioni 10 tangu mwaka wa 2017.
Wakiongozwa na Katibu mkuu wa Muungano wa UASU Constantine Wasonga, Wahadhiri hao walilalamika kwamba serikali imeshindwa kutekeleza awamu ya pili ya nyongeza ya mishahara ya mwaka wa 2021 hadi 2025.
“Tumetoa onyo kwa serikali hadi tarehe 17 mwezi huu wa Septemba iwe imetimiza matakwa yetu yote ya mkataba wa makubaliano wa CBA mwaka wa 2017 wa shilingi bilioni 10 na pia tufanye mazungumzo na serikali kuhusu mkataba wa makubaliano wa malipo CBA wa mwaka wa 2021 hadi 2025”, alisema Wasonga.
Wahadhari hao walishikilia kwamba kuna masuala mengi ibuka ambayo serikali haijatimiza na imekuwa ikitoa ahadi kila mara, wakisema kwamba ni lazima serikali kupitia Wizara ya Elimu nchini kutimiza ahadi hizo kwa wakati.
Taarifa ya Mwahoka Mtsumi