News

Wahudumu wa Tuktuk Malindi washinikiza uhamisho wa Trafiki.

Published

on

Wahudumu wa sekta ya Tuktuk mjini Malindi kaunti ya Kilifi wamelalamika kuhangaishwa na maafisa wa trafiki mjini humo licha ya kutimiza vigezo hitajika vya kuwaruhusu kuhudumu barabarani.

Mwenyekiti wa wahudumu hao kaunti ya Kilifi Abdhalla Mwangi alisema kuwa serikali inafaa kukifanyia mabadiliko kitengo hicho ili kutatua mzozo uliopo baina ya wahudumu hao na maafisa wa trafiki.

Mwangi alisistiza haja ya swala hilo kuangaziwa kwa kina kutokana na kile alichodai kuwa hali hiyo imeathiri pakubwa sekta hiyo kiuchumi.

“Hawa trafiki hawaturidishi kabisa, Malindi ulikuwa ni mji mzuri ambao unautulivu saa hii unaweza kubebwa na dereva, atazunguka kitambo afike mahali anaenda yaani hata wewe mwenyewe utamuonea huruma, hawa jamaa wamekuwa niusumbufu saa hii sio oparesheni”, alisema Mwangi.

 

   .

Maafisa wa trafiki katika barabara za humu nchini(picha kwa hisani)

Mwangi aidha alibainisha kuwa licha ya kuwasilisha ombi la kutaka uhamisho wa maafisa wa trafiki waliohudumu kwa muda mrefu mjini humo, hakuna hatua zozote zilizochukuliwa na serikali kufikia sasa

“Nilizungumza na serikali kuwaomba kwamba kuna maafisa wa trafiki hapa kwetu ambao hawana nidhamu za kikazi na wanagonganisha madereva na serikali, tukaomba serikali hawa watu wahamishwe, na mpaka sasa hatujaona hatua yeyote ambayo imefanyika”,aliongeza Mwangi

Taarifa ya Mwanahabari wetu

Leave a Reply

Your email address will not be published. Required fields are marked *

Trending

Exit mobile version