Connect with us

News

Wahudumu wa Tuktuk Malindi washinikiza uhamisho wa Trafiki.

Published

on

Wahudumu wa sekta ya Tuktuk mjini Malindi kaunti ya Kilifi wamelalamika kuhangaishwa na maafisa wa trafiki mjini humo licha ya kutimiza vigezo hitajika vya kuwaruhusu kuhudumu barabarani.

Mwenyekiti wa wahudumu hao kaunti ya Kilifi Abdhalla Mwangi alisema kuwa serikali inafaa kukifanyia mabadiliko kitengo hicho ili kutatua mzozo uliopo baina ya wahudumu hao na maafisa wa trafiki.

Mwangi alisistiza haja ya swala hilo kuangaziwa kwa kina kutokana na kile alichodai kuwa hali hiyo imeathiri pakubwa sekta hiyo kiuchumi.

“Hawa trafiki hawaturidishi kabisa, Malindi ulikuwa ni mji mzuri ambao unautulivu saa hii unaweza kubebwa na dereva, atazunguka kitambo afike mahali anaenda yaani hata wewe mwenyewe utamuonea huruma, hawa jamaa wamekuwa niusumbufu saa hii sio oparesheni”, alisema Mwangi.

 

   .

Maafisa wa trafiki katika barabara za humu nchini(picha kwa hisani)

Mwangi aidha alibainisha kuwa licha ya kuwasilisha ombi la kutaka uhamisho wa maafisa wa trafiki waliohudumu kwa muda mrefu mjini humo, hakuna hatua zozote zilizochukuliwa na serikali kufikia sasa

“Nilizungumza na serikali kuwaomba kwamba kuna maafisa wa trafiki hapa kwetu ambao hawana nidhamu za kikazi na wanagonganisha madereva na serikali, tukaomba serikali hawa watu wahamishwe, na mpaka sasa hatujaona hatua yeyote ambayo imefanyika”,aliongeza Mwangi

Taarifa ya Mwanahabari wetu

Continue Reading
Click to comment

Leave a Reply

Your email address will not be published. Required fields are marked *

News

Wazee wa Kaya wanataka bunge kupitisha sheria kudhibiti mauaji ya wazee

Published

on

By

Muungano wa Wazee wa Kaya kaunti ya Kilifi umeitaka serikali kuu kupitia bunge la kitaifa kubadilisha sheria ya mwaka wa 1926 kuhusu uchawi ili kuwezesha utamaduni kudhibiti mauaji ya wazee yanayoendelea kushuhudiwa kaunti ya Kilifi.

Wakiongozwa na Stanley Kahindi Kiraga wamesema kuwa sheria hiyo imechangia pakubwa mauaji ya wakongwe Kilifi kutokana na swala kuwa haitambui uwepo wa uchawi na jinsi ya kuudhibiti.

Kiraga sasa anasema ni sharti sheria hiyo iondolewe au ifanyiwe ukarabati bungeni hali itayopelekea uchawi kudhibitiwa kupitia mila na utamaduni.

“Vijana wanaowaua wazee wakiwasingizia kuwa wachawi wanazidi kuongezeka na kwa sababu hakuna sheria ya moja kwa moja ya kuwashtaki na kuwafunga” amesema Kiraga akieleza kusikitishwa kwake na ongezeko la magenge ya vijana wanaolipwa kutekelezwa mauaji ya wazee kwa shutuma za uchawi.

Taarifa ya Hamis Kombe

Continue Reading

News

Mahakama ya Kilifi yaanzisha upya kesi ya ulaghai wa pesa

Published

on

By

Mahakama ya Kilifi imeanzisha upya kesi ya mwanaume mmoja anayekabiliwa na shtaka la ulaghai wa pesa.

Hii ni baada ya Mwanaume huyo kwa jina Samuel Ngonyo, kuachiliwa kwa dhamana hapo awali lakini alikosa kudhuhuria vikao Mahakamani hali iliyopelekea kesi hiyo kuanzishwa upya.

Hakimu mkuu wa Mahakama hiyo Charles Obulutsa aliagiza jamaa huyo kuzuliwa rumande baada ya agizo la kukamatwa kwake kuidhinishwa na Mahakama baada ya jamaa huyo kupuuza vikao vya Mahakama vya awali.

Kabla ya agizo hilo, Mahakama ilielezwa kwamba mnamo tarehe tofauti kati ya mwezi Septemba hadi Oktoba mwaka 2021 katika maeneo la Ganze kaunti ya Kilifi kwa kutumia njia ya ulaghai, mshukiwa alichukua pesa taslimu shilingi elfu 50 ya mlalamishi Grace Sidi Katana.

Mahakama ilielezwa zaidi kwamba mshukiwa alitekeleza kitendo hicho baada kumdanganya Mlalamishi kwamba yeye ni Mwandishi na afisa wa kazi za umma hivyo angemsaidia Moses Katana mtoto wa mlalamishi kupata kazi ya serikali.

Kesi hiyo itaendelea mnamo tarehe 13 mwezi Agosti mwaka huu.

Taarifa ya Mwanahabari wetu

Continue Reading

Trending