News

Ujenzi wa Barabara ya Kuelekea Timbo za Jaribuni Kuanza

Published

on

Kikao cha kutafuta mwafaka kuhusu mzozo uliyoshuhudiwa kati ya wakaazi wa eneo la Jaribuni kaunti ya Kilifi na wawekezaji wa timbo za eneo hilo uliyosababisha kufungwa kwa barabara, kilifanyika ramsi.

Kikao hicho kilichoongozwa na Waziri wa madini na Uchumi samawati nchini Ali Hassan Joho kilijumuisha pia wawekezaji wa timbo hizo na wenyeji kama hatua moja wapo ya kuibuka na mwafaka.

Kikao hicho ambacho pia kilihudhuriwa na Gavana wa Kilifi Gedion Mung’aro kimeshuhudia kuanzishwa kwa mradi wa ujenzi wa barabara zinazoelekea katika timbo za eneo hilo la Jaribuni.

Japo barabara hizo zimesalia kufungwa kufuatia maandamano yaliyoshuhudiwa ya wenyeji wakilalamikia uchafuzi wa mazingira, ubovu wa barabara pamoja na kupuuzwa kwa miradi ya maendeleo, huenda sasa mwafaka wa mzozo huo ukapatikana

Leave a Reply

Your email address will not be published. Required fields are marked *

Trending

Exit mobile version