Connect with us

News

Ujenzi wa Barabara ya Kuelekea Timbo za Jaribuni Kuanza

Published

on

Kikao cha kutafuta mwafaka kuhusu mzozo uliyoshuhudiwa kati ya wakaazi wa eneo la Jaribuni kaunti ya Kilifi na wawekezaji wa timbo za eneo hilo uliyosababisha kufungwa kwa barabara, kilifanyika ramsi.

Kikao hicho kilichoongozwa na Waziri wa madini na Uchumi samawati nchini Ali Hassan Joho kilijumuisha pia wawekezaji wa timbo hizo na wenyeji kama hatua moja wapo ya kuibuka na mwafaka.

Kikao hicho ambacho pia kilihudhuriwa na Gavana wa Kilifi Gedion Mung’aro kimeshuhudia kuanzishwa kwa mradi wa ujenzi wa barabara zinazoelekea katika timbo za eneo hilo la Jaribuni.

Japo barabara hizo zimesalia kufungwa kufuatia maandamano yaliyoshuhudiwa ya wenyeji wakilalamikia uchafuzi wa mazingira, ubovu wa barabara pamoja na kupuuzwa kwa miradi ya maendeleo, huenda sasa mwafaka wa mzozo huo ukapatikana

Continue Reading
Click to comment

Leave a Reply

Your email address will not be published. Required fields are marked *

News

Seneta Madzayo amuonya Inspekta jenerali wa Polisi.

Published

on

By

Seneta wa kaunti ya Kilifi Stewart Madzayo amemtaka inspekta jenerali wa polisi nchini Douglas Kanja kuhakikisha maandamano ya vijana wa rika la Gen z tarehe 25 mwezi juni 2025 hayashuhudii umwagikaji damu.

Madzayo ambaye pia ni kiongozi wa wachache katika bunge la seneti alimtaka Inspekta Kanja kuhakikisha maafisa wa polisi wanawalinda waandamanaji badala ya kuwadhuru.

Akizungumza eneo la Mzambarauni-Mtwapa eneo bunge la Kilifi Kusini, Madzayo alidokeza kuwa maandamano hayo yatakuwa ya amani akikumbusha vijana hao wa Gen Z kuhakikisha wanadumisha amani wakati wa maandamano hayo.

“Tumeskia tarehe 25 kutakuwa na maandamano ya amani, nataka kumwambia inspekta jenerali Kanja, tafadhali watoto wetu watakuwa katika maandamano ya amani kwa hivyo usijaribu hata kidogo kutumia polisi vibaya kuweza kuumiza watoto wetu”, alisema Madzayo.

Kwa upande wake mbunge wa eneo hilo Ken Chonga aliwaomba viongozi wa kanisa nchini kuombea taifa kutokana na visa vya mauaji na utekeji nyara vinavyoshuhudiwa nchini.

“Tumekuwa na changamoto kubwa sana kati ya upinzani na serikali hali ya maafa ikiingia, haya yote ambayo yanaendelea sa hii yote sababu ni siasa, langu ni kusihi kwanza kanisa tunahitaji maombi yenu”, alisistiza Chonga.

Maandamano hayo ya GEN Z yanatarajiwa kufanyika tarehe 25 mwezi juni 2025 kukumbuka vijana waliopoteza maisha wakati wa maandamano ya kupinga mswada wa fedha mwezi juni mwaka 2024.

Taarifa ya Joseph Jira

Continue Reading

News

Joho atangaza kuwania urais siku zijazo

Published

on

By

Waziri wa madini na masuala ya bahari nchini Hassan Ali Joho, alidokeza kwamba katika siku zijazo eneo la Pwani litatoa rais wa taifa la Kenya.

Waziri Joho aliwataka wakaazi wa Pwani kutojiingiza katika mivutano ya kisiasa na mirengo mingine ya kisiasa nchini, akisema ni wakati mwafaka wa wapwani kuungana na kujipanga kisiasa.

Waziri Joho alisema mtu ambaye alikuwa na nafasi nzuri ya kushikilia wadhfa huo wa kitaifa aliyekuwa ni Marehemu Karisa Maitha lakini ndoto hiyo bado ipo, akiweka wazi kwamba anamezea mate kiti hicho katika siku zijazo.

“Mara ya kwanza nilifikia kama kuna mpwani anaweza kuwa rais ilikuwa ni marehemu Karisa, lakini mimi hiyo ndoto bado niko nayo na nina imani iko siku bado hapa Pwani kuzaa rais. Siku moja wataskia rais Hassan na nikujipanga”, alisema Joho.

Joho alisisitiza haja ya wapwani kujipanga kisiasa ili kuwa katika nafasi nzuri ya kuvuna kwenye ngazi ya kitaifa pamoja na kuwa rahisi kwa eneo la Pwani kuwania kiti hicho na kutangaza rais wa Kenya katika siku zijazo.

Taarifa ya Mwahoka Mtsumi

Continue Reading

Trending