News

Serikali kutumia AI katika utoaji wa huduma kwa umma

Published

on

Waziri wa utumishi wa Umma nchini Geoffrey Ruku anasema serikali inaangazia kuwianisha mishahara ya watumishi wa umma na kukumbatia mageuzi ya kidijitali, ikiwa ni pamoja na matumizi ya mfumo wa akili mnemba (AI), ili kuboresha ufanisi katika utoaji huduma.

Akizungumza wakati wa hafla ya kufunga toleo la 44 la michezo ya shirika la michezo ya huduma za kiraia nchini (KECOSO) katika uwanja wa Moi mjini Embu, Ruku aliekiri kuwepo tofauti za malipo katika sekta ya umma na kusema mageuzi yanaendelea.

Waziri huyo aliwapongeza watumishi wa umma kwa kujitolea katika utendakazi wa, akisema Kenya ina mojawapo ya wafanyakazi wenye nguvu zaidi katika utumishi wa umma barani afrika.

Ruku pia aliangazia mkakati wa serikali wa kidijitali-kwanza unaoongozwa na wizara ya mawasiliano, akisema mfumo wa AI na zana za kidijitali zitakuwa muhimu katika kubadilisha utendakazi.

Taarifa ya Joseph Jira

Leave a Reply

Your email address will not be published. Required fields are marked *

Trending

Exit mobile version