News

Oyuu: Fedha za Shule Zisambazwe kwa Wakati

Published

on

Katibu mkuu wa Chama cha kutetea maslahi ya walimu nchini (KNUT) Collins Oyuu ameitaka serikali kuu kuharakisha mchakato wa kusambaza fedha za kufadhili masomo shuleni.

Oyuu amesema mtaala mpya wa elimu nchini CBC utafaulu iwapo shule zitapokea fedha hizo kwa wakati na ziwe za kutosha.

Katibu huyo amedokeza kwamba walimu wakuu katika shule hizo wanapitia wakati mgumu kuendesha shughuli za shule baada ya serikali kujikokota katika usambazaji wa hela shuleni.

Wakati huo huo amesema baadhi ya walimu wakuu wamekuwa wakijikuta na matatizo ya afya ya akili kutokana na changamoto hizo.

Leave a Reply

Your email address will not be published. Required fields are marked *

Trending

Exit mobile version