Connect with us

News

Oyuu: Fedha za Shule Zisambazwe kwa Wakati

Published

on

Katibu mkuu wa Chama cha kutetea maslahi ya walimu nchini (KNUT) Collins Oyuu ameitaka serikali kuu kuharakisha mchakato wa kusambaza fedha za kufadhili masomo shuleni.

Oyuu amesema mtaala mpya wa elimu nchini CBC utafaulu iwapo shule zitapokea fedha hizo kwa wakati na ziwe za kutosha.

Katibu huyo amedokeza kwamba walimu wakuu katika shule hizo wanapitia wakati mgumu kuendesha shughuli za shule baada ya serikali kujikokota katika usambazaji wa hela shuleni.

Wakati huo huo amesema baadhi ya walimu wakuu wamekuwa wakijikuta na matatizo ya afya ya akili kutokana na changamoto hizo.

Continue Reading
Click to comment

Leave a Reply

Your email address will not be published. Required fields are marked *

News

Kampuni ya Simba Cement yafungwa, Kaloleni

Published

on

By

Serikali ya kaunti ya Kilifi kwa ushirikiano na Wizara ya Madini imesitisha rasmi shughuli zote za uchimbaji madini zinazotekelezwa na kampuni ya Simba Cement eneo la Kaloleni kaunti ya Kilifi.

Agizo hilo limetolewa na Gavana wa kaunti ya Kilifi Gideon Mung’aro pamoja na Waziri wa madini na raslimali za uchumi wa bahari nchini Ali Hassan Joho, wakisema kampuni hiyo imeshindwa kufuata sheria za mazingira na haiwafaidi wakaazi wa eneo hilo.

Viongozi hao walisema shughuli za uchimbaji wa kampuni hiyo zimekuwa zikiathiri mazingira na wakazi wa maeneo ya karibu, huku wakiahidi kwamba serikali haitavumilia ukosefu wa uwajibikaji unaotishia afya na maisha ya wananchi.

Walisisitiza kwamba kampuni hiyo haitaruhusiwa kuendelea na shughuli zake hadi pale itakapokidhi masharti yote ya kisheria na kuthibitisha kwamba haileti madhara kwa binadamu wala mazingira.

“Hii kampuni wacha nikuambie waziri haisadii wananchi wa Kilifi kwa chochote waziri, na leo hii watu wa kambe ribe mnisikize na mnisikize kwa makini, vile nilifanya Jaribuni ndivyo nitakavyofanya leo, kuanzia kesho asubuhi na nitawafuata na barua kesho mwelezeni mwajiri wenu kwamba hii kampuni tumeifunga na nitawafuata na barua”, alisema Gavana Mung’aro.

Hatua hii iliungwa mkono na baadhi ya viongozi wa jamii na wanaharakati wa mazingira, wakisema kuwa ni wakati wa kuwajibisha wawekezaji wanaokiuka haki za wananchi kwa msingi ya maendeleo.

Simba Cement, ambayo imekuwa ikihusishwa na miradi mikubwa ya ujenzi, sasa inalazimika kukabiliwa na masharti mapya kabla ya kurejelea shughuli zake za kawaida.

Taarifa ya Elizabeth Mwende

Continue Reading

News

Kanja aagizwa kuwasilisha stakabadhi za Polisi kwa NPSC

Published

on

By

Huduma ya kitaifa ya polisi nchini NPS iliagizwa kukabidhi orodha ya malipo ya polisi na kazi zote zinazohusiana na raslimali za umma kwa Tume ya kitaifa ya huduma ya polisi nchini NPSC.

Agizo hilo lilitolewa na Kamati ya bunge la kitaifa kuhusu uhasibu wa umma inayoongozwa na Mbunge wa Butere Tindi Mwale ambayo ilimuagiza Inspekta Jenerali wa polisi Douglas Kanja kutekeleza agizo hilo mara.

Kulingana na kamati hiyo, hatua hiyo itapunguza uhasama uliopo kati ya taasisi hizo mbili za umma huku ikimtaka Kanja kuhakikisha pia anawasilisha orodha ya mishahara sawa na kuruhusu tume hiyo kutekeleza majuku yake kwa mujibu wa katiba.

Hata hivyo Inspekta Jenerali wa polisi nchini Douglas Kanja aliahidi kutekelezwa kwa maagizo hayo huku mkurugenzi mkuu wa Tume ya huduma ya kitaifa ya polisi nchini NPSC Peter Lelei akiahidi kuandikia Kamati hiyo barua kuhakikisha iwapo maagizo hayo yametekelezwa.

Kanja alikuwa aliitwa mbele ya kamati hiyo kufuatia ripoti iliyotolewa na Mkaguzi mkuu wa hesabu za serikali Magaret Nyakang’o iliyoashiri kwamba NPSC haijaweza kutekeleza majukumu yake kwa kunyimwa stakabadhi muhimu.

Taarifa ya Mwahoka Mtsumi

Continue Reading

Trending