Business
Msongamano Miritini–Jomvu Wazidisha Hasara kwa Wahudumu wa Matatu
Wahudumu wa matatu katika barabara ya kutoka kaloleni Mombasa wanasema Biashara zao zimedorora kutokana na msongamano ambao unashuhudiwa katika eneo la miritini hadi jomvu.
Kulingana na wahudumu hao masaa wanayotumia njiani ni mengi hali ambayo inawafanya kukadiria hasara bidhaa zao zikiharibika.
Wanasema wanatumia fedha nyingi kuagiza bidhaa mbalimbali ila zinaharibikia njiani kutokana na msongamano huo.
“ tuna kaa kwa zaidi ya saa tano barabarani kufuatia msongamnao wa magari hasa malori ambayo hayasongi kabisa jambo amabyo linatusababishia hasara.
“Tunnaomba aliyepewa ujenzi wa barabara hii kuikamilisha haraka iwezekanavyo.”.
Aidha wamemtaka mwanakandarasi aliyepewa ujenzi wa barabaya hiyo kuikamilisha ili kupunguza msongamano huo kwani wanategemea Biashara kujikimu kimaisha hivyo kuendelea kuchelesha kukamilishwa kwa ujenzi huo kunazidi kuwasababishia hasara.