News

Miili iliyosalia Shakahola kuzikwa na Serikali

Published

on

Huenda serikali ikalazimika kuizika miili ya watu waliofariki dunia eneo la Shakahola, Magarini kaunti ya Kilifi baada ya zoezi la kuitambua miili hiyo kusitishwa.

Waziri wa usalama wa ndani, Kipchumba Murkomen alisema kuwa miili hiyo itazikwa katika sehemu moja na kisha sehemu hiyo kutengwa kama hifadhi ya kumbukumbu kwa waathiriwa.

Murkomen alisema kuwa zoezi hilo limekwama kutokana na familia nyingi kutojitokeza kuitambua miili hiyo akisema kuwa huenda ikawa miili mingi iliyopo kwa sasa sio ya watu waliokuwa wakaazi na wenyeji wa Kilifi.

“Hii miili sio ya Kilifi kaunti pekee bali Kenya nzima, Baringo, Vihiga, Siaya, Kisumu, maeneo hayo yote na sasa jamaa za watu hao hawajui kama watu waliopotea ni kweli walienda Shakahola na wakakufia huko, ndio maana hawajitokezi ili kufanyia sampuli za vinasaba”, alisema Murkomen

Kufuatia hilo Murkomen alihoji kuwa huenda serikali ikatumia njia mbadala kukamilisha zoezi hilo

Taarifa ya Hamis Kombe

Leave a Reply

Your email address will not be published. Required fields are marked *

Trending

Exit mobile version