News
Miili iliyosalia Shakahola kuzikwa na Serikali

Huenda serikali ikalazimika kuizika miili ya watu waliofariki dunia eneo la Shakahola, Magarini kaunti ya Kilifi baada ya zoezi la kuitambua miili hiyo kusitishwa.
Waziri wa usalama wa ndani, Kipchumba Murkomen alisema kuwa miili hiyo itazikwa katika sehemu moja na kisha sehemu hiyo kutengwa kama hifadhi ya kumbukumbu kwa waathiriwa.
Murkomen alisema kuwa zoezi hilo limekwama kutokana na familia nyingi kutojitokeza kuitambua miili hiyo akisema kuwa huenda ikawa miili mingi iliyopo kwa sasa sio ya watu waliokuwa wakaazi na wenyeji wa Kilifi.
“Hii miili sio ya Kilifi kaunti pekee bali Kenya nzima, Baringo, Vihiga, Siaya, Kisumu, maeneo hayo yote na sasa jamaa za watu hao hawajui kama watu waliopotea ni kweli walienda Shakahola na wakakufia huko, ndio maana hawajitokezi ili kufanyia sampuli za vinasaba”, alisema Murkomen
Kufuatia hilo Murkomen alihoji kuwa huenda serikali ikatumia njia mbadala kukamilisha zoezi hilo
Taarifa ya Hamis Kombe
News
Kenya kuzindua utalii wa anga (Astro-tourisim)

Kenya itakuwa mwenyeji wa uzinduzi wa utalii wa anga(Astro-tourisim) katika kaunti ya Samburi Septemba 7, 2025, ikiwa ni sehemu ya juhudi za kuimarisha na kubadilisha aina za utalii nchini.
Uzinduzi huo unaendana sambamba na tukio la mwezi kupatwa maarufu kama Blood moon ambapo litaanza saa mbili na nusu usiku wa septemba 7, 2025, na kudumu kwa dakika 82.
Mpango huu wa kipekee unalenga kuifanya Kenya kuwa kivutio kikuu cha wapenzi wa sayansi ya anga na wasafiri wa kimataifa wanaopenda maajabu ya siri.
Kwa mujibu wa shirika la Magical Kenya, tajriba hii ya anga inalenga kutumia mazingira ya kipekee ya nchi kufungua ukurasa mpya na endelevu wa utalii.
Waziri wa utalii na wanyama pori Rebecca Miano atakuwa mgeni rasmi akiandamana na wageni wa kimataifa katika hafla hiyo itakayofanyika katika Sopa Lodge kwenye hifadhi ya kitaifa ya Samburu.
Taarifa ya Joseph Jira
News
Serikali kukabiliana na magenge ya uhalifu nchini

Waziri wa Usalama Kipchumba Murkomen ameonya kuhusu kuongezeka kwa magenge ya wahalifu nchini.
Akizungumza katika kongamano la Jukwaa la Usalama kaunti ya Vihiga, Waziri Murkomen alitoa wito kwa inspekta jenerali wa polisi kutuma vikosi zaidi vya dharura eneo hilo ili kuwasambaratisha wahalifu hao.
Magenge ya wahalifi yamekuwa yakiripotiwa kuhangaisha usalama na maisha ya wakaazi katika sehemu mbali mbali nchini ikiwepo kaunti za hapa Pwani.
Kwa upande wake gavana wa kaunti ya Kilifi Gedion Mung’aro aliahidi kushirikiana kwa karibu na maafisa wa usalama kukomesha magenge ya wahalifu yanayowahangaisha wakaazi maarufu mawoza.
Akizungumza mjini Malindi katika kaunti ya Kilifi kwenye mkutano na vijana wa eneo hilo, gavana Mung’aro alisema serikali yake haitawavumilia vijana waliopotoka kimaadili wanaoendelea kuwahangaisha wananchi.
Wakati huohuo aliwaonya baadhi ya maafisa wa kaunti wanaowahangaisha wakaazi hususan wahudumu wa bodaboda.
Taarifa ya Joseph Jira.
-
Sports23 hours ago
Ndoto ya Harambee Stars ya kufuzu Kombe la Dunia 2026 Yagonga mwamba baada ya kupigwa 3-1 na Gambia Kasarani
-
Sports23 hours ago
Sinner na Alcaraz Wakutana Tena Fainali ya US Open Baada ya Muitaliano Kufuzu Fainali ya Tano Mfululizo ya Grand Slam
-
News3 hours ago
IEBC yasistiza usalama kwenye maandalizi ya uchaguzi mkuu