News
Migos: Serikali yajipanga kwa mpito wa Junior Secondary Januari, 2026
Waziri wa Elimu Julius Migos Ogamba alisema serikali ya kitaifa imejiandaa kikamilifu kwa mpito wa wanafunzi kuingia Sekondari ya Juu (Junior Secondary), Januari 2026.
Akizungumza katika Chuo Kikuu cha Embu, Waziri Migos alisema kuwa mikakati imewekwa kuhakikisha wanafunzi wa Gredi ya 10 hawakosi masomo wanapojiunga na shule hizo.
Aliongeza kwamba serikali imewekeza katika ujenzi wa miundombinu, hasa madarasa ili kuhakikisha shule zinakuwa tayari kwa mapokezi ya wanafunzi hao.
Hata hivyo, wadau wa elimu walielezea wasiwasi wao kuhusu utayari wa serikali, hasa katika masuala ya miundombinu ya shule, ufadhili wa wanafunzi, upatikanaji wa vitabu, maabara, mafunzo kwa walimu na uratibu wa mikondo mitatu ya masomo kama ilivyopangwa.
“Kama serikali, tumejiandaa kupokea watoto wetu kutoka Gredi ya 9 hadi 10. Wanafunzi wameshaanza kuchagua kati ya mikondo mitatu ya masomo na shule, na tumehakikisha zoezi hilo linakamilika kwa ufasaha,” alisema Waziri Migos.
Taarifa ya Elizabeth Mwende.