News
Mboko: Dhulma za kijinsia dhidi ya watoto lazima zikomeshwe
Mbunge wa Likoni Bi Mishi Mboko amewakosoa baadhi ya wakaazi wa eneo bunge hilo kwa madai ya kukosa kuchukulia kwa uzito kesi za dhulma za kijinsia dhidi ya watoto.
Bi Mboko alisema vitendo hivyo vinakiuka haki za mtoto na wenyeji wanapaswa kuwa mstari wa mbele kuhakikisha wanadhibiti visa hivyo.
Bi Mboko ambaye alikuwa akizungumza katika eneo bunge lake la Likoni, alisema kuna haja ya wakaazi kuripoti visa hivyo kwa asasi za kiuslama ili washukiwa wa visa hivyo wakabiliwe kisheria.
“Hizi kesi za Femicide na GBV kwa nini ushahidi upotee polisi, ati evidence hakuna na mtoto ameletwa akiwa yuko katika zile hali na kila kitu alafu ati ushahidi unapotea, please handle these cases with the heart of humanity’’, alisema Bi Mboko.
Vilevile, aliwahimiza maafisa wa polisi kuwajibika vilivyo pindi kesi hizo zinaporipotiwa kwao.
Wakati huo huo, alitoa wito kwa wenyeji wa Likoni kushirikiana na vitengo vya usalama ili kudhibiti visa vya watoto wenye umri mdogo kujiungiza katika uhalifu na kuhakikisha watoto hao wanapelekwa katika vituo vya kurekebisha tabia.
Taarifa ya Janet Mumbi