Business

KPA kushirikiana na kaunti ya Siaya kibiashara

Published

on

Halmashauri ya bandari Kenya (KPA) pamoja na serikali ya kaunti ya Siaya zimeahidi kushirikiana kwa karibu kuimarisha miundomsingi ya usafiri na biashara katika ukanda wa Ziwa Victoria.

Katika kikao cha viongozi wa pande zote mbili kilichofanyika jijini Mombasa, viongozi hao walijadili miradi ya miundomsingi ya baharini inayolenga kufungua fursa mpya za uwekezaji na mageuzi ya kiuchumi kwa wakazi wa maeneo ya Ziwa Victoria.

Mkurugenzi mkuu wa KPA nahodha William Ruto alithibitisha kuwa usanifu wa kivuko cha Usenge utakamilika ndani ya wiki mbili, huku ikiahidi kushirikiana na Kenya Shipyards Limited kuhakikisha ujenzi wake unakamilika kwa wakati.

Aidha, Ruto alieeleza utayari wa mamlaka hiyo kushirikiana na serikali ya kaunti ya Siaya kuhakikisha miradi hiyo inaendana na vipaumbele vya eneo hilo.

Ruto aliongeza kuwa miradi hiyo inalenga kuchochea uwekezaji, kuongeza nafasi za ajira na kuleta mabadiliko ya kiuchumi katika ukanda wa ziwa.

Kwa upande wake, gavana wa kaunti ya Siaya James Orengo alieleza kuridhishwa na ushirikiano huo, akimpongeza nahodha Ruto kwa uongozi wake wa vitendo akisema kuwa miradi hiyo inaleta matumaini mapya kwa wakazi wa Siaya na ukanda mzima wa Ziwa Victoria.

Taarifa ya Mwanahabari wetu

Leave a Reply

Your email address will not be published. Required fields are marked *

Trending

Exit mobile version