News
Mwashako, amtaka Waziri Duale kuwataja wanaohusika na sakata ya SHA
Mbunge wa Wundanyi Danson Mwashako alielezea kukerwa na madai ya ufisadi yanayoendelea kushughudiwa humu nchini hasa kwenye Bima ya afya ya jamii nchini SHA.
Mwashako alisema ni jambo la kusikitisha kuona viongozi wakijadili suala hilo bila kuchukua hatua zozote mwafaka, hali ambayo inachangia wananchi wengi kutokuwa na imani na viongozi wao.
Mwashako ambaye pia ni Mwenyekiti wa Muungano wa wabunge wa Pwani alimtaka Waziri wa Afya nchini Aden Duale kuwataja hadharani wale wanaohusika na sakata za ufisadi kwenye bima hiyo, akisisitiza kwamba hatua hiyo itasaidia kuimarisha utendakazi wake kama Waziri.
“Kila siku pesa zinapotea, tuseme tu ukweli mimi kama Mwashako inanisumbua sana ndio maana nasema sisi kama viongozi hata mbinguni hatutaenda na siku zote nimekuwa nikimwambia Duale kama uchunguzi imefanywa basi asiogope awataje hadharini wale wetu walihusika na kuiba pesa ya SHA kwa sababu ukiangalia E-Citizen pesa pia inaibwa kila siku”, alisema Mwashako.
Wakati huo huo, alivilaumu vitengo vya usalama nchini hasa Idara ya ujasusi nchini NIS na Idara ya upelelezi wa jinai nchini DCI kwa kuzembea kuwajibikia majukumu yao huku wananchi wakikabiliwa na madhara kutokana na hali hiyo.
Kauli yake ilijiri huku Kamati ya Afya katika bunge la kitaifa ikiongozwa na Mwenyekiti wake ambaye pia ni mbunge wa Seme Dkt James Nyikal ikiilaumu Wizara ya Afya nchini kwa kuharibu utekelezaji wa uzidunzi wa Mamlaka ya Afya ya jamiI SHA.
Viongozi wa kamati hiyo walisema changamoto hizo zinaathiri huduma za hospitali mbalimbali za umma nchini sawa na kuwakosesha wagonjwa wengi huduma muhimu za afya.
Taarifa ya Mwahoka Mtsumi