News

Wazee wa Kaya walaumu mgawanyiko wa maandalizi ya Chendachenda

Published

on

Mungano wa Wazee wa Kaya za Mijikenda umeelezea kusikitishwa na hatua ya serikali ya kaunti ya Kilifi ya kupanga kuandaa tamasha za tamaduni za jamii ya Mijikenda za Chendachenda katika chuo kikuu cha Pwani mbali na maelewano ya kuandaa tamasha hilo kaunti ya Kwale.

Katika taarifa yao kwa vyombo vya habari Muungano huo ulitaja hatua hiyo kama ya kuwakosea heshima Wazee wa Kaya.

Wazee hao walidai kwamba hatua ya serikali ya kaunti ya Kilifi chini ya gavana Gedion Mung’aro inania ya kutenganisha jamii ya Mijikenda mbali na kuwaunganisha.

Aidha walisisitiza kuchukua msimamo na kuandaa tamasha hilo katika Kaya ya Mtswakara kaunti ya Kwale na yeyote atakayeenda kinyume na maamuzi ya Wazee hao atakumbana na laana za wazee.

Waliitaka serikali ya kaunti ya Kilifi kuomba msamaha kutokana na hatua hiyo.

Taarifa ya muungano wa wazee wa Kaya kwa vyombo vya habari

Awali tamasha hiyo iliandaliwa katika kaunti ya Kilifi na ilitarajiwa kuandaliwa katika kaunti tofauti kati ya kaunti sita za Pwani, kulingana na makubaliano ya jamii ya Mijikenda.

Hatua hii imeonekana kusababisha mgawanyiko miongoni mwa viongozi wa Kaya na viongozi wa siasa eneo la Pwani

Taarifa ya Joseph Jira

Leave a Reply

Your email address will not be published. Required fields are marked *

Trending

Exit mobile version