News

Kaunti ya Lamu yakabiliwa na changamoto ya nguvu za umeme

Published

on

Kaunti ya Lamu inaendelea kushuhudia changamoto ya nguvu za umeme ambayo inaendelea kuathiri utoaji wa huduma katika idara mbali mbali katika kaunti hiyo.

Gavana wa kaunti hiyo Issa Timamy alisema kaunti hiyo imelazimika kutumia mitambo ya kunasa miale ya jua maarufu sola ili kutoa huduma mbali mbali kwa wakaazi wa kaunti hiyo.

Kulingana na gavana Timamy hali hiyo imechangiwa na gharama za juu za umeme sawa na kupotea kwa nguvu za umeme mara kwa mara.

Timamy pia alisema visima vikuu vya kusambaza maji katika chemichemi ya maji ya milima ya bahari eneo la Shela vinatumia umeme wa sola kuvuta maji ili yafike majumbani.

Gavana huyo alidokeza kuwa mashine ya kubadilisha maji ya bahari kuwa maji ya kunywa eneo la Mkokoni pia hutumia umeme wa sola na pia taa za barabarani maeneo yote ya Lamu.

Taarifa ya Joseph Jira

Leave a Reply

Your email address will not be published. Required fields are marked *

Trending

Exit mobile version