Connect with us

News

Kanja aagizwa kuwasilisha stakabadhi za Polisi kwa NPSC

Published

on

Huduma ya kitaifa ya polisi nchini NPS iliagizwa kukabidhi orodha ya malipo ya polisi na kazi zote zinazohusiana na raslimali za umma kwa Tume ya kitaifa ya huduma ya polisi nchini NPSC.

Agizo hilo lilitolewa na Kamati ya bunge la kitaifa kuhusu uhasibu wa umma inayoongozwa na Mbunge wa Butere Tindi Mwale ambayo ilimuagiza Inspekta Jenerali wa polisi Douglas Kanja kutekeleza agizo hilo mara.

Kulingana na kamati hiyo, hatua hiyo itapunguza uhasama uliopo kati ya taasisi hizo mbili za umma huku ikimtaka Kanja kuhakikisha pia anawasilisha orodha ya mishahara sawa na kuruhusu tume hiyo kutekeleza majuku yake kwa mujibu wa katiba.

Hata hivyo Inspekta Jenerali wa polisi nchini Douglas Kanja aliahidi kutekelezwa kwa maagizo hayo huku mkurugenzi mkuu wa Tume ya huduma ya kitaifa ya polisi nchini NPSC Peter Lelei akiahidi kuandikia Kamati hiyo barua kuhakikisha iwapo maagizo hayo yametekelezwa.

Kanja alikuwa aliitwa mbele ya kamati hiyo kufuatia ripoti iliyotolewa na Mkaguzi mkuu wa hesabu za serikali Magaret Nyakang’o iliyoashiri kwamba NPSC haijaweza kutekeleza majukumu yake kwa kunyimwa stakabadhi muhimu.

Taarifa ya Mwahoka Mtsumi

Continue Reading
Click to comment

Leave a Reply

Your email address will not be published. Required fields are marked *

News

Mahakama kuu yatupilia mbali ombi la Gachagua

Published

on

By

Mahakama kuu imetupilia mbali ombi la pili la aliyekuwa Naibu Rais Rigathi Gachagua la kutaka jopo la majaji watatu wanaosikiliza kesi ya kupinga kubanduliwa wake mamlakani kuzuiliwa kuskiza kesi hiyo. 

Gachagua alisema kwamba majaji hao watatu akiwemo Jaji Eric Ogola, Anthony Mrima na Fridah Mugambi wanafaa kuondolewa kwenye kesi hiyo kwa misingi kwamba uteuzi wao haujazingatia sheria.

Mahakama hiyo ilitupilia mbali ombi hilo, na kusema kwamba jopo hilo la majaji watatu liliteuliwa na Jaji mkuu Martha Koome kwa kuambatana na sheria na kanuni za idara ya Mahakama.

Mahakama imeshikilia kwamba jopo hilo la majaji wa Mahakama kuu litaendelea kusikiliza kesi hiyo hadi wakati wa kutoa uamuzi kwa kuzingatia sheria, na kanuni za idara ya Mahakama pamoja na Katiba ya Kenya.

Mahakama hiyo pia ilitupilia mbali ombi la Mwanaharakati Fredrick Mula ambaye alitaka kubadilishwa kuwa mlalamishi katika kesi nne za kuondolewa mashtaka dhidi ya aliyekuwa Naibu Rais Rigathi Gachagua ambazo alikuwa amewasilisha awali na kisha kutaka kujiondoa.

Taarifa ya Mwahoka Mtsumi

Continue Reading

News

Wazee wa Kaya wanataka bunge kupitisha sheria kudhibiti mauaji ya wazee

Published

on

By

Muungano wa Wazee wa Kaya kaunti ya Kilifi umeitaka serikali kuu kupitia bunge la kitaifa kubadilisha sheria ya mwaka wa 1926 kuhusu uchawi ili kuwezesha utamaduni kudhibiti mauaji ya wazee yanayoendelea kushuhudiwa kaunti ya Kilifi.

Wakiongozwa na Stanley Kahindi Kiraga wamesema kuwa sheria hiyo imechangia pakubwa mauaji ya wakongwe Kilifi kutokana na swala kuwa haitambui uwepo wa uchawi na jinsi ya kuudhibiti.

Kiraga sasa anasema ni sharti sheria hiyo iondolewe au ifanyiwe ukarabati bungeni hali itayopelekea uchawi kudhibitiwa kupitia mila na utamaduni.

“Vijana wanaowaua wazee wakiwasingizia kuwa wachawi wanazidi kuongezeka na kwa sababu hakuna sheria ya moja kwa moja ya kuwashtaki na kuwafunga” amesema Kiraga akieleza kusikitishwa kwake na ongezeko la magenge ya vijana wanaolipwa kutekelezwa mauaji ya wazee kwa shutuma za uchawi.

Taarifa ya Hamis Kombe

Continue Reading

Trending