News

Kampeni ya Chanjo kwa watoto yafanikiwa nchini

Published

on

Wizara ya afya nchini imesema kufikia sasa watoto milioni 3.3 wamepokezwa chanjo ya surua kati ya watoto milioni 6.5 waliolengwa.

Ripoti ya wizara hiyo pia iliongeza kuwa watoto milioni 12.1 wamepokea chanjo ya homa ya matumbo kati ya waliolengwa milioni 19.2.

Vile vile ripoti hiyo ilisema kuwa zaidi ya watoto elfu nne ambao walikuwa hawajapokea chanjo yeyote awali sasa wamefanikiwa kuchanjwa.

Wizara hiyo iliongeza kuwa kampeni hiyo ya kitaifa ya chanjo iliyoanza tarehe 5 Julai, 2025, imepokelewa vyema na wazazi, viongozi wa dini, walezi, wahudumu wa afya na wakenya kwa jumla.

Wizara hiyo ilishauri wazazi na walezi kuhakikisha watoto wao wanapewa chanjo hiyo ikiwa zimesalia siku tatu pekee kabla kampeni kuu kukamilika.

Chanjo hizo zimeidhinishwa na shirikala afya dunia WHO na zimethibitshwa kuwa salama, bora na huokoa maisha.

Waziri wa afya Aden Duale alisema serikali imejitolea kuhakikisha hakuna mtoto atakayepoteza maisha kwa ugonjwa unaoweza kuzuilika kwa Chanjo.

Taarifa ya Joseph Jira

Leave a Reply

Your email address will not be published. Required fields are marked *

Trending

Exit mobile version