Rais wa Uganda Yoweri Museveni mwenye umri wa miaka 81 ameidhinishwa na tume ya uchaguzi ya nchi hiyo kugombea nafasi ya urais katika uchaguzi mkuu wa mwaka ujao.
Katika hotuba yake ya uteuzi, Museveni aliishukuru Tume hiyo kwa kuidhinisha ugombea wake. Pia alikipongeza chama tawala cha National Resistance Movement (NRM) kwa kumwamini na kumchagua kupeperusha bendera ya urais katika uchaguzi ujao.
Museveni alisema kwamba wana misukumo miwili mikuu, msukumo namba moja ni kwa tabaka la kati na wawekezaji kutoka nje kubadilisha kabisa Uganda kutoka nchi ya kipato cha chini hadi nchi ya kipato cha kati kuelekea nchi ya kwanza ya ulimwengu.
Museveni, ambaye alitawala nchi hiyo ya Afrika mashariki kwa karibu miongo minne, anatafuta muhula wa saba wa kuchaguliwa baada ya kuwasilisha ugombea wake, Museveni anatarajiwa kuzungumza na wafuasi wake katika mkutano wa hadhara katika uwanja wa uhuru nje kidogo ya mji mkuu Kampala.
Mpinzani wake mkuu katika uchaguzi wa urais wa 2021 mwanamuziki aliyegeuka kuwa mwanasiasa Robert Kyagulanyi almaarufu Bobi Wine atateuliwa siku ya Jumatano, 24.9.2025.
Vyama vinne vya kisiasa tayari vilijiondoa katika kinyang’anyiro cha urais, ikiwa ni pamoja na Democratic Party, chama kongwe zaidi cha kisiasa nchini Uganda na Political Front for Freedom [PFF] kilichoanzishwa na Dk. Kizza Besigye, mkosoaji mkubwa wa Museveni.
Kwa mara ya pili mfululizo nchi hiyo itafanya uchaguzi bila mgombea urais mara nne, Dk. Besigye kuonekana kwenye karatasi ya kura.
Alikamatwa mwaka jana akiwa Kenya na hadi sasa bado yuko kizuizini kwa mashtaka ya uhaini, makossa ambayo ameyakanusha yote.
Hata hivyo, wakosoaji walisema Museveni alitawala Uganda kwa mkono wa chuma tangu achukue madaraka kama kiongozi wa waasi mwaka 1986 na ameshinda kila uchaguzi tangu wakati huo.
Wakati wa uchaguzi uliopita wa 2021, alishinda kwa 58% wakati mpinzani wake wa karibu, Bobi Wine alishika nafasi ya pili kwa 34%.
Nchi hiyo itafanya uchaguzi mkuu ujao Januari 12. 2026.
Taarifa ya Elizabeth Mwende