Sports
Bado Hawajamaliza Kulipa Starlets Asema Rais Wa FKF
Rais wa Shirikisho la mchezo wa soka nchini Hussein Mohammed amefichua kwamba wamelipa badhi ya marupurupu kwa kikosi cha soka kwa akina dada Harambee Starlets.
Hata hivyo akizungumza na kituo kimoja nchini Mohammed amefichua kwamba bado hawajalipa marurupu ya kikosi hicho mechi za kirafiki dhidi ya Ivory Coast mwezi April,Rais huyo akiongezea kwamba kazi ya kulipa wachezaji hao ni ya Serikali kupitia wizara ya michezo na wala si ya Shirikisho la soka nchini.
“Tumelipa badhi ya marupurupu kulikuwepo na tatizo upande wa wizara ila swala hilo sasa limetatuliwa akina dada hao watapokea pesa zao ikiwemo ya Cecafa nchini Tanzania.”
Alipoulizwa iwapo kama ndiyo chanzo ya badhi ya wachezaji kujiondoa kwenye kambi ya Starlets Hussein amesema wanasubiri ripoti kutoka kwa kocha wa timu hiyo Beldine Odemba.
Starlets wako nchini Tanzania mashindano Afrika Mashariki na kati CECAFA.