Sports
Bado Hawajamaliza Kulipa Starlets Asema Rais Wa FKF

Rais wa Shirikisho la mchezo wa soka nchini Hussein Mohammed amefichua kwamba wamelipa badhi ya marupurupu kwa kikosi cha soka kwa akina dada Harambee Starlets.
Hata hivyo akizungumza na kituo kimoja nchini Mohammed amefichua kwamba bado hawajalipa marurupu ya kikosi hicho mechi za kirafiki dhidi ya Ivory Coast mwezi April,Rais huyo akiongezea kwamba kazi ya kulipa wachezaji hao ni ya Serikali kupitia wizara ya michezo na wala si ya Shirikisho la soka nchini.
“Tumelipa badhi ya marupurupu kulikuwepo na tatizo upande wa wizara ila swala hilo sasa limetatuliwa akina dada hao watapokea pesa zao ikiwemo ya Cecafa nchini Tanzania.”
Alipoulizwa iwapo kama ndiyo chanzo ya badhi ya wachezaji kujiondoa kwenye kambi ya Starlets Hussein amesema wanasubiri ripoti kutoka kwa kocha wa timu hiyo Beldine Odemba.
Starlets wako nchini Tanzania mashindano Afrika Mashariki na kati CECAFA.
Sports
Mchezaji Tenesi Alcaraz Bingwa Tena

Mchezaji Tenesi anayeorodheshwa wa Pili duniani kwa sasa Carlos Alcaraz raia wa Uhispania ameweza kuandikisha rekodi mpya baada ya kushinda taji la pili kombe la Queens Cup Title baada ya kumlaza Jiri Licheka raia wa Czech kwa seti za 7-5, 6-7 (5/7), 6-2 kabila ya finali ya Wimblendon.
Nyota huyo raia wa Uhispania alimzidi mwenzake kwenye fainali baada ya kuonyesha makali tokea mwanzo huku mchezaji huyo anayeorodheshwa wa 30 akikubali kichapo hicho kwa muda lisali 2 na dakika 10.
Mwanatenesi huyo tayari ana mataji matano baada ya kuzishinda fainali za French Open,Rome Open,Monte Carlo na Rotherdam mwaka huu wa 2025.
Mwamba huyo hajapoteza katika mashindano fainali 18 mpaka sasa tangu fainali za Barcelona Open April 20.
Sports
Kilabu Ya Oklahoma City Thunder Ndiyo Mabingwa NBA

Kilabu ya Oklahoma ndiyo mabingwa wa mchezo wa mpira vikapu marekani NBA mwaka 2025 Fainali kali iliopigwa Jumapili hii.
Hii ni baada ya vijana hao kuwanyamazisha Indiana Pacers alama 103-91 katika raundi ya 7 ya mechi hizo na kaundikisha historia mpya.
Hili ni taji lao la kwanza tangu kuondoka kutoka mji Seattle mwaka 2008.