News

Rais Ruto, Amteua Ethekon kuwa Mwenyekiti wa IEBC

Published

on

Rais William Ruto amemteua Erastus Edung Ethekon kuwa Mwenyekiti wa Tume huru ya uchaguzi na mipaka nchini IEBC na makamishna 6 wa tume hiyo ili kufanikisha shughuli za uchaguzi nchini.

Katika chapisho la gazeti rasmi la serikali, Rais Ruto amezingatia kipengele cha 250 ibara ya pili {a} ya Katiba ya Kenya na mwongozo wa uteuzi wa makamishna wa sehemu ya 5 na 7 na kutekeleza jukumu hilo.

Katika chapisho hilo lililotiwa saini na Mkuu wa utumishi wa umma nchini Felix Koskei, Rais amezingatia muongozo wa Katiba na kuwateua makamishna 6 wa tume hiyo akiwemo Ann Njeri Nderitu kutoka kaunti ya Nyandarua, Moses Alutalala Mukhwana kutoka kaunti ya Kakamega na Mary Karen Sorobit kutoka kaunti ya Uasin Gishu.

Wengine ni pamoja na Hassan Noor Hassan kutoka kaunti ya Mandera, Francis Odhiambo Aduol kutoka kaunti ya Kisumu pamoja na Fahima Araphat Abdallah kutoka kaunti ya Lamu.

Sasa majina ya makamishna hao na Mwenyekiti mpya wa IEBC yatawasilishwa bungeni kupigwa msasa na kuidhinishwa kabla ya kuapishwa ili kuanza majukumu yao ya kikazi.

Leave a Reply

Your email address will not be published. Required fields are marked *

Trending

Exit mobile version