News
Rais Ruto, Amteua Ethekon kuwa Mwenyekiti wa IEBC

Rais William Ruto amemteua Erastus Edung Ethekon kuwa Mwenyekiti wa Tume huru ya uchaguzi na mipaka nchini IEBC na makamishna 6 wa tume hiyo ili kufanikisha shughuli za uchaguzi nchini.
Katika chapisho la gazeti rasmi la serikali, Rais Ruto amezingatia kipengele cha 250 ibara ya pili {a} ya Katiba ya Kenya na mwongozo wa uteuzi wa makamishna wa sehemu ya 5 na 7 na kutekeleza jukumu hilo.
Katika chapisho hilo lililotiwa saini na Mkuu wa utumishi wa umma nchini Felix Koskei, Rais amezingatia muongozo wa Katiba na kuwateua makamishna 6 wa tume hiyo akiwemo Ann Njeri Nderitu kutoka kaunti ya Nyandarua, Moses Alutalala Mukhwana kutoka kaunti ya Kakamega na Mary Karen Sorobit kutoka kaunti ya Uasin Gishu.
Wengine ni pamoja na Hassan Noor Hassan kutoka kaunti ya Mandera, Francis Odhiambo Aduol kutoka kaunti ya Kisumu pamoja na Fahima Araphat Abdallah kutoka kaunti ya Lamu.
Sasa majina ya makamishna hao na Mwenyekiti mpya wa IEBC yatawasilishwa bungeni kupigwa msasa na kuidhinishwa kabla ya kuapishwa ili kuanza majukumu yao ya kikazi.
News
Kilabu Ya Liverpool Yamnasa Frimpong

Beki wa kilabu ya Bayern Leverkusen Jeremie Frimpong ni rasmi amejiunga na mabingwa wa ligi kuu Uingereza Liverpool.
Beki huyo mholanzi amejiunga na The Reds kwa pauni milioni 29.5 na amemwaga wino mkataba wa miaka 5 na kilabu hio kuchukua nafasi ya Alexander Trent Arnaold ambaye ni rasmi amejiunga na kilabu ya Real Madrid.
Mholanzi huyo anakua mchezaji wa tano kuvalia jezi ya kilabu hio wengine akiwa ni pamoja na Cody Gakpo,Virgil Van Dijik,Ryan Gravenberch.
Nyota huyo ambaye pia amekuwa akiwindwa na Manchester United na miamba wa Uhispania Rea Madrid amesema kwamba alichagua kilabu hiyo kwani ndio inaendana na mipango yake ya mbeleni kama mchezaji akiahidi kushinda mataji na miamba hao wa Uingereza.
News
Shughuli za Masomo Zatatizwa katika Shule ya Msingi ya Arabuko Sokoke

Shughuli za masomo katika shule ya msingi ya Arabuko Sokoke eneo la Kakuyuni kaunti ya Kilifi zilitatizika mapema siku ya Ijumaa baada ya Wazazi kuandamana wakilalamikia usimamizi mbaya wa shule hiyo.
Wakaazi hao wamemtaka Mwalimu kuu wa shule hiyo kupewa uhamisho kwani ameonyesha wazi kushindwa kusimamia shughuli za masomo katika shule hiyo.
Wakiongozwa na Joyce Mbuche, Wazazi hao wamesema Mwalimu mkuu wa shule hiyo amekosa kuwa wazi kwa wazazi kuhusu suala la matumizi ya Fedha ya shule hiyo pamoja na kutokuwa muadilifu kazini.
Wazazi hao hata hivyo wamesema Mwalimu mkuu huyo amekuwa hawalipi mishahara walimu ambao wanasimamiwa na wazazi katika shule hiyo huku baadhi ya wanafunzi wakikosa kusajiliwa katika mfumo wa KEMIS.