News
UEFA:Inter Ndaani Ya Fainali
Miamba wa Italia kilabu ya Inter Milan imekua ya kwanza kutinga awamu ya fainali kilabu bingwa Ulaya baada ya kunyuka FC Barcelona kichapo cha magoli 4-3 na jumla ya magoli 7-6 uwanjani San Siro jana usiku.
Inter walitangulia kucheka na wavu kunako dakika ya 21 kupitia kwa mshambulizi Lautaro Martinez dakika ya 21 kabla ya kiungo Hakan Çalhanoğlu kuweka kambani goli la pili dakika ya 46 kipindi cha kwanza.
Hata hivyo Barcelona walirejea kwa moto wa radi kipindi cha pili na kusawazisha la kwanza kunako dakika ya 54 kupitia beki Erick Garcia naye mshambulizi Dani Olmo akiweka la pili dakika ya 60.
Licha ya Barcelona kuchukua uongozi dakika ya 87 kupitia kwa mahambulizi Raphinha, Inter walisawazisha kupitia kwa beki Fransisco Acerbi dakika ya 93 na kupeka mechi hiyo kwenye muda wa ziada ama extra time ukipenda.
Kiungo mshambulizi na nguvu mpya Davide Fratessi alifunga goli la ushindi la Inter dakika ya 99 na kupeleka kilabu hiyo kwenye fainali Alianz Arena Mei 31.
Hii leo ni zamu ya mabingwa wa ufaransaPSG kutifua kivumbi na Arsenal uwanjani Parc de prince.