News
UEFA:Inter Ndaani Ya Fainali

Miamba wa Italia kilabu ya Inter Milan imekua ya kwanza kutinga awamu ya fainali kilabu bingwa Ulaya baada ya kunyuka FC Barcelona kichapo cha magoli 4-3 na jumla ya magoli 7-6 uwanjani San Siro jana usiku.
Inter walitangulia kucheka na wavu kunako dakika ya 21 kupitia kwa mshambulizi Lautaro Martinez dakika ya 21 kabla ya kiungo Hakan Çalhanoğlu kuweka kambani goli la pili dakika ya 46 kipindi cha kwanza.
Hata hivyo Barcelona walirejea kwa moto wa radi kipindi cha pili na kusawazisha la kwanza kunako dakika ya 54 kupitia beki Erick Garcia naye mshambulizi Dani Olmo akiweka la pili dakika ya 60.
Licha ya Barcelona kuchukua uongozi dakika ya 87 kupitia kwa mahambulizi Raphinha, Inter walisawazisha kupitia kwa beki Fransisco Acerbi dakika ya 93 na kupeka mechi hiyo kwenye muda wa ziada ama extra time ukipenda.
Kiungo mshambulizi na nguvu mpya Davide Fratessi alifunga goli la ushindi la Inter dakika ya 99 na kupeleka kilabu hiyo kwenye fainali Alianz Arena Mei 31.
Hii leo ni zamu ya mabingwa wa ufaransaPSG kutifua kivumbi na Arsenal uwanjani Parc de prince.
News
Kesi dhidi ya Mackenzie na washukiwa wenzake 38 inaendelea Mahakamani

Kesi dhidi ya mhubiri tata Paul Mackenzie na washukiwa wenzake 38 kuhusu ukatili na ukiukaji wa haki za watoto inaendelea kusikizwa katika mahakama ya watoto ya Tononoka kaunti ya Mombasa mbele ya hakimu mkuu Nelly Chepchirchir, mashahidi 3 wakishuhudia.
Shahidi wa 47 ambaye ni mtaalamu wa tiba ya watoto kutoka kituo cha watoto cha Malindi kaunti ya Kilifi, ameeleza mahakama hali dhaifu ya kisaikolojia ya mvulana mdogo aliyekuwa miongoni mwa watoto 8 waliookolewa kutoka kwenye msitu wa Shakahola.
Amesema mazungumzo ya usaidizi na uchunguzi wa kitabibu yaliwasaidia watoto kukabiliana na msongo wa mawazo.
Mtaalamu huyo amesema pia baada ya tathmini yake ya kitaalamu, alipendekeza mazingira salama ya malezi ya msaada kwa mtoto huyo kwasababu alikuwa na hofu ya kurudishwa Shakahola.
Pia amehitaji msaada wa kisaikolojia wa mara kwa mara kwa sababu alikuwa na wasiwasi kuhusu familia yake waliopotea.
Naye shashidi wa 48 na 49 Zadock Odiaho na mkewe Deborah wameeleza jinsi mwanao Wilfred Mulama na mkewe walivyowatoa watoto wao wawili shuleni na kujaribu kuwashawishi watoto wa majirani kuwa kwenda shule ni dhambi.
Wameiambia Mahakama kwamba baadae Mulama alikamatwa na kuhukumiwa kifungo cha mwaka mmoja cha uangalizi kwa kushindwa kuwapeleka watoto shule akiwa na wajibu wa kuripoti kwa polisi kila wiki lakini kabla ya kifungo hicho kukamilika, alitorokea Shakahola na familia yake yote.
Wameeleleza Mahakama kwamba Mulama aliuza vitu vyake vyote kabla ya kutoweka na kuhamia Shakahola.
Wameiambia Mahakama kuwa waliwahi kuwasiliana na wachunguzi wa kesi za Shakahola, waliomwambia kuwa walikuwa wameokoa mjukuu wake msituni baada ya kupigwa hadi kushindwa kutembea.
News
Washukiwa wa uhalifu wakamatwa maeneo ya Likoni kaunti ya Mombasa

Mafisa kutoka kituo cha polisi cha Vijiweni eneo la Likoni kaunti ya Mombasa, usiku wa kuamkia leo wamewakamata wanaume watatu wanaoshukiwa kuwa wahalifu katika maeneo ya Likoni na sehemu za Kaunti ya Kwale.
Kulingana na ripoti za polisi, watuhumiwa hao, Abubakar Juma Koba mwenye umri wa miaka 17, Ali Bakari mwenye umri wa miaka 17 na Mohamed Ruwa mwenye umri wa miaka 18 ni wanachama wa kundi la vijana wanaotumia mapanga, ambao wanashutumiwa kwa kuwahangaisha wakazi katika maeneo ya Mwaweche Magulani na Dongo Kundu.
Watuhumiwa walikamatwa wakati wa doria ya usiku kufuatia taarifa za kijasusi.
Wengine watano walifanikiwa kutoroka.