News
Zoezi la kutoa chanjo kung’oa nanga Julai 5
Wizara ya Afya imetangaza kampeni ya kutoa Chanjo bila malipo kote nchini katika juhudi za kukabiliana na maradhi ya ukambi, Homa ya tumbo na Surua.
Zoezi hilo la siku 10 linatarajiwa kuanza Julai 5 mwaka huu hadi Julai 14.
Afisa wa masuala ya Chanjo kaunti ya Kilifi Christine Mataza, na mwenzake wa Afya ya Umma Amos Ndenge wamesema zaidi ya watoto elfu 200 walio chini ya umri wa miaka mitano watapokea chanjo ya ukambi na Surua.
Aidha wamesema kwamba zaidi ya Chanjo elfu 200 za Homa ya Matumbo itapeyanwa kwa zaidi ya watoto elfu 600 wa kati ya miezi tisa hadi miaka 14 katika kaunti ya Kilifi.
Chanjo hizo ambazo hutolewa kila baada ya miaka mitano, mwaka huu itaendeshwa katika sehemu za masoko, na shule, kinyume na miaka ya nyuma ambapo zoezi hilo lilikuwa likitekelezwa nyumba hadi nyumba.
Homa ya tumbo husababishwa na matumizi ya maji machafu na Mazingira machafu huku Kenya ikiwa ni Taifa la tano barani Africa kuanzisha Chanjo mpya ya kukabiliana na Huma ya tumbo, ukambi na Surua barani Afrika
Taarifa ya Eric Ponda